Category Archives: BIASHARA NA UJASIRIAMALI

BIASHARA LEO; Changamoto Ya Kupanga Bei Na Jinsi Ya Kukabiliana Nayo.

By | June 15, 2015

Kupanga bei kwenye biashara ni changamoto kubwa sana unayotakiwa kuifanyia kazi vizuri kama kweli unataka kupata mafanikio makubwa kupitia biashara unayofanya. Watu wengi wamekuwa wakifikiria kwamba ukishusha bei basi utapata wateja wengi sana. Huu sio ukweli kuuza vitu kwa bei ya chini kunaweza kuwa kikwazo kwako kupata wateja wengi zaidi (more…)

Vitu muhimu vya kuzingatia ili kukuza biashara yako.

By | June 15, 2015

Peter Drucker, aliyekuwa mtaalamu wa usimamizi kwenye biashara, aliwahi kusema kwamba kwa kuwa lengo la biashara ni kutengeneza wateja, biashara yoyote ina majukumu mawili tu ya msingi; masoko na ubunifu. Vitu hivi viwili ndio vinaleta faida kwenye biashara, vingine vyote vinaleta gharama. Leo katika makala hii ya kona ya mjasiriamali (more…)

BIASHARA LEO; Mtazamo Wa Kuvuna Na Mtazamo Wa Kujenga.

By | June 13, 2015

Katika biashara kuna mitazamo miwili mikubwa, mtazamo wa kwanza ni wa kuvuna, na mtazamo wa pili ni wa kujenga. Mtazamo wa kuvuna. Hapa ni pale ambapo mfanyabiashara anaangalia ni kitu gani anakipata sasa. Yeye anafikiria kuvuna tu na hivyo anapoipata fursa anaitumia kwa uhakika. Na kama hakuna njia ya kuvuna (more…)

BIASHARA LEO; Umuhimu Na Jinsi Ya Kujenga Uaminifu Kwa Wateja Wako.

By | June 12, 2015

Biashara ni uaminifu, kama hakuna uaminifu hakuna biashara. Kama bado unafanya biashara kwa mazoea yale ya zamani kwamba biashara ni kuwaibia watu, usiendelee kusoma makala hii maana tutakavyojadili hapa hutavielewa. Badala yake fungua makala za nyuma kwenye kipengele hiki cha BIASHARA LEO na uanze kujifunza yale muhimu kwanza. Sasa twende (more…)

BIASHARA LEO; Kutojali Kwako Kunavyokuletea Hasara Kwenye Biashara.

By | June 11, 2015

BIASHARA LEO; Kutojali Kwako Kunavyokuletea Hasara Kwenye Biashara. Jana nilikuwa kwenye ofisi moja, mama mmoja akatoka kwenda kutoa fedha kwa njia ya simu na kununua vocha pia. Baada ya muda alirudi akiwa amekamilisha zoezi lake na kutaka kuingiza vocha kwenye simu. Alipoangalia akakuta amepewa vocha mara mbili ya alizoagiza. Alinunua (more…)

BIASHARA LEO; Sehemu Mbili Anazokwenda Mteja Wako Unazotakiwa Kuzijua.

By | June 10, 2015

Unapokuwa kwenye biashara, jukumu lako kubwa ni kumjua mteja wako kuliko hata anavyojijua wewe mwenyewe. Labda sio, lakini cha msingi lazima umjue mteja wako vizuri. Changamoto nyingi za biashara zinaanza pale mfanyabiashara anaposhindwa kumjua mteja wake vizuri na hivyo anashindwa kwenda naye vizuri kwenye biashara yake. Kama unasema huna haja (more…)

BIASHARA LEO; Njia Tatu Muhimu Za Kukuza Biashara Yako.

By | June 9, 2015

Unafanyia kazi haya unayojifunza kwenye kipengele hiki cha BIASHARA LEO? Kama unafanyia tushirikishe kwenye maoni hapo chini ni jinsi gani biashara yako inabadilika. Na kama hufanyii kazi tuambie ni kwa nini? Yote tunayojifunza kwenye kipengele hiki sio vitu vya kufurahia kusoma, bali ni vitu unatakiwa kufanya. Unasoma kitu hapa na (more…)

BIASHARA LEO; Umuhimu Wa Mafunzo kwa wafanyakazi wako na jinsi ya kuyapata.

By | June 8, 2015

Wafanyakazi wako ni watu muhimu sana kwenye biashara yako. Hawa ni watu ambao wataiwezesha biashara yako kufanikiwa au kushindwa. Wafanyabiashara wengi wamekuwa hawalipi uzito eneo la wafanyakazi. Wengi wamekuwa wakiajiri wafanyakazi kwa sababu tu ni rahisi kuwalipa na hawatawasumbua, hivyo wafanyakazi hawa wanakuwa hawana ujuzi wowote wa biashara. Kwa kufanya (more…)

Jinsi ya kutumia wateja wako kama sehemu ya kutangaza biashara yako.

By | June 8, 2015

Linapokuja swala la kutangaza biashara, watu hufikiria matangazo kwenye vyombo vikubwa vya habari, kupata tangazo wakati wa taarifa ya habari, ambapo watu wengi wanaangalia. Au kudhamini michezo inayofuatiliwa na wengi. Au kuweka bango kubwa kwenye eneo ambalo watu wengi wanapita. Hizi zote ni njia nzuri za kutangaza biashara yako, ila (more…)

BIASHARA LEO; Usihofu Kama Watu Hawakuelewi.

By | June 6, 2015

Moja ya changamoto za kuwa mjasiriamali ni kwamba watu wengi hawatakuelewa. Kama unayafanyia kazi haya mambo ambayo unajifunza hapa kila siku, watu wengi hawawezi kukuelewa. Usiogope pale hali hii inapotokea, maana ndio umeanza kuuelewa ujasiriamali. Watu wengi hawawezi kukuelewa kwa sababu walitegemea ufanye biashara kama wanavyofanya wao. Ufungue biashara yako (more…)