2856; Ishi kila siku kama ndiyo siku yako ya mwisho.

By | October 26, 2022

2856; Ishi kila siku kama ndiyo siku yako ya mwisho. Huwa tunaona tuna muda mwingi, mpaka pale tunapokuja kugundua muda wetu umeisha. Ni rahisi kujiambia utafanya kesho, kwa kuwa umezoea kuziona kesho nyingi. Lakini ipo siku ambayo hutaiona kesho uliyopanga. Ubaya ni huwezi kuijua siku hiyo ni ipi. Lakini uhakika (more…)

#SheriaYaLeo (359/366); Jiweke kwenye uwanja wa kifo.

By | October 25, 2022

#SheriaYaLeo (359/366); Jiweke kwenye uwanja wa kifo. Tangu enzi na enzi, majenerali wa majeshi wamekuwa wakitafuta njia ya kuwasukuma wanajeshi wao kupambana kwa kila namna ili kupata ushindi. Wapo ambao wamekuwa wakitunia maneno ya hamasa ili kuwahamasisha wanajeshi wao kupambana. Maneno hayo yamekuwa na mafanikio kiasi lakini nguvu yake huwa (more…)

2855; Wewe ni miujiza.

By | October 25, 2022

2855; Wewe ni miujiza. Kupatikana kwako ni tukio la miujiza mikubwa. Kukutana kwa wazazi wako, lilikuwa tukio ambalo hakuna aliyelitegemea. Wazazi wako kuamua kufanya mapenzi siku ambayo mimba yako ilitungwa pia ni tukio ambalo huenda lisingetokea. Kama mmoja wao angekuwa amesafiri au kuumwa, siku hiyo zoezi hilo lisingefanyika. Katika mbegu (more…)

#SheriaYaLeo (358/366); Epuka ukuaji wa kiroho feki.

By | October 24, 2022

#SheriaYaLeo (358/366); Epuka ukuaji wa kiroho feki. Changamoto kubwa tunayokabiliana nayo kwenye zama hizi ni wengi kushindwa kujua njia sahihi za ukuaji wa kiroho. Lengo la dini lilipaswa kuwa njia ya watu kupata ukuaji wa kiroho. Lakini kwa zama hizi, dini zimeshindwa kuwasaidia watu kwenye hilo. Badala yake zimewajaza hofu (more…)

2854; Ng’ang’ana mpaka ufanikiwe.

By | October 24, 2022

2854; Ng’ang’ana mpaka ufanikiwe. Wanaofanikiwa na wanaoshindwa wote huanza sawa. Huwa wanaanza na ndoto kubwa walizonazo. Kisha wanachukua hatua kwenye ndoto hizo. Katika kuchukua huko hatua huwa wanakutana na changamoto na vikwazo mbalimbali. Na hapa ndipo wanaofanikiwa na wanaoshindwa wanapotofautiana. Wanaoshindwa huwa wanakata tamaa haraka pale wanapokutana na vikwazo na (more…)

#SheriaYaLeo (357/366); Ujinga wa kiwango cha juu.

By | October 23, 2022

#SheriaYaLeo (357/366); Ujinga wa kiwango cha juu. Binadamu tunazaliwa, kuishi na kufa. Hivyo ndivyo maisha yamekuwepo tangu enzi na enzi na ndiyo imewezesha dunia kuendelea kuwepo. Viumbe wanaokufa wanatoa nafasi kwa wengine wanaozaliwa. Baadhi ya watu wanatafuta teknolojia ya kurefusha maisha au kuondoa kabisa kifo. Huu ni ujinga wa hali (more…)

2853; Ipokee kila siku kwa upendo.

By | October 23, 2022

2853; Ipokee kila siku kwa upendo. Upendo ndiyo nguvu kuu inayoiendesha dunia. Upendo ndiyo imani kuu inayowaleta watu wote pamoja. Upendo una nguvu kubwa ya kuleta mapinduzi kwenye maisha ya kila mtu. Ili kufanikiwa, unapaswa kuipokea kila siku kwa upendo mkuu. Unapaswa kuongozwa na upendo kila siku. Upendo unapaswa kuanzia (more…)

#SheriaYaLeo (356/366); Tumia kifo kuziondoa tofauti.

By | October 22, 2022

#SheriaYaLeo (356/366); Tumia kifo kuziondoa tofauti. Kifo ni moja ya vitu vinavyotuleta mahali pamoja wote. Ni kitu kinachotufanya wote kuwa sawa kwa sababu mwisho wa siku wote tutakufa. Haijalishi tofauti zetu kwenye maisha, wote njia yetu ni moja, kifo. Yote tunayobaguana nayo hayana tofauti kwenye kifo. Kwa kujua hatima hii (more…)

2852; Kuwa mtumwa wa tabia nzuri.

By | October 22, 2022

2852; Kuwa mtumwa wa tabia nzuri. Tulipokuwa watoto, tulikuwa watumwa wa hisia. Tuliendeshwa na hisia na kila mara kufanya yale tuliyojisikia kufanya. Tumekuwa watu wazima na sasa tumekuwa watumwa wa tabia. Tumejenga tabia na sasa tabia zinatujenga. Mambo mengi tunayofanya tunayafanya kwa tabia, kwa jinsi ambavyo tumezoea kufanya. Ubaya wa (more…)

2851; Uwezo tayari upo, tofauti ni matumizi.

By | October 21, 2022

2851; Uwezo tayari upo, tofauti ni matumizi. Unga wa ngano, unaweza kutengeneza mandazi, chapati, mkate, keki na vingine vingi. Uwezo wote huo tayari upo ndani ya unga, ila matokeo ya mwisho yanategemea jinsi ambacho uwezo huo umetumiwa. Kadhalika kwetu binadamu, chochote ambacho wanadamu wengine wameshaweza kufanya, hata wewe una uwezo (more…)