#SheriaYaLeo (355/366); Jua yaliyo muhimu.

By | October 21, 2022

#SheriaYaLeo (355/366); Jua yaliyo muhimu. Tuna malengo ya kufikia, miradi ya kukamilisha na mahusiano ya kuboresha. Chochote tunachofanya kwa wakati wowote ule kinaweza kuwa ndiyo kitu cha mwisho kwetu kufanya. Hivyo tunapaswa kuhakikisha kila tunachofanya ndiyo kilicho muhimu zaidi na kuweka juhudi zetu zote kwenye kitu hicho. Kwa utambuzi huu (more…)

2850; Ushindi kila siku.

By | October 20, 2022

2850; Ushindi kila siku. Sisi binadamu huwa tunapenda sana ushindi. Ndiyo maana huwa tupo tayari kushindana hata kwenye mambo yasiyokuwa na tija. Ile hali ya kushinda tu inatufanya tujisikie vizuri. Lakini sasa, maisha huwa hayatupi ushindi kirahisi. Huwa yanatupa kila aina ya vikwazo na changamoto ili tu tusipate ushindi. Na (more…)

#SheriaYaLeo (354/366); Jichukulie umezaliwa upya.

By | October 20, 2022

#SheriaYaLeo (354/366); Jichukulie umezaliwa upya. Pale unapopitia magumu sana kwenye maisha yako na kuona kama yamefika tamati, ila ukaweza kuyavuka, unapaswa kutumia hali hiyo kuishi kwa tija zaidi. Jichukulie kama mtu uliyezaliwa upya, ambaye umepata nafasi nyingine ya maisha baada ya kushindwa kutumia vizuri nafasi ya awali. Kwa kujichukulia umezaliwa (more…)

2849; Watu na matokeo.

By | October 19, 2022

2849; Watu na matokeo. Kama kiongozi, una mambo hayo makubwa mawili ya kuzingatia. Una watu unaowaongoza na kuwasimamia na una matokeo ambayo unapaswa kuyazalisha. Haya mawili yanakwenda pamoja kwa sababu ni watu ndiyo wanaozalisha matokeo unayoyataka. Na hapo ndipo penye mtego mkubwa kwenye uongozi, kwa sababu unahitaji mlinganyo mzuri sana (more…)

#SheriaYaLeo (353/366); Kuwa na haraka na matamanio.

By | October 19, 2022

#SheriaYaLeo (353/366); Kuwa na haraka na matamanio. Unapokuwa na muda mwingi wa kufanya kitu, huwa inakuwa rahisi kuahirisha kufanya kitu hicho, kwa kujiambia utafanya kesho. Tunapokuwa na muda mwingi huwa tunaishia kuupoteza kwa usumbufu na mambo yasiyokuwa na tija kwetu. Inakuwa vigumu kuweka umakini wetu wote kwenye yaliyo muhimu na (more…)

2848; Lengo, Sifa, Maboresho.

By | October 18, 2022

2848; Lengo, Sifa, Maboresho. Hivyo ni vitu vitatu vinavyoweza kukufanya kuwa kiongozi bora kabisa kutokea. Ni vitu unavyopaswa kuvifanya kwako na kwa wote unaowaongoza. Kwanza unaanza na lengo, nini hasa unachotaka kupata? Au matokeo gani yanapaswa kupatikana? Lengo lazima liwe wazi na kueleweka na wote wanaohusika. Na liweze kuelezewa kwa (more…)

#SheriaYaLeo (352/366); Kuona kitu kwa mara ya mwisho.

By | October 18, 2022

#SheriaYaLeo (352/366); Kuona kitu kwa mara ya mwisho. Kama binadamu tungekuwa tunaishi milele, maisha yangepoteza maana. Ni ufupi wa maisha ndiyo unatufanya tuyathamini na kufanya yale yenye tija. Lakini wakati mwingine huwa tunajisahau na kuzoea vitu, kwa kuona vipo muda wote. Ili kuondoka kwenye mazoea haya na kuvithamini vitu, tunapaswa (more…)

2847; Kukaa kati.

By | October 17, 2022

2847; Kukaa kati. Dunia inaendeshwa kwa upacha, pande mbili zinazotofautiana. Usiku na mchana. Jinsia ya kike na ya kiume. Juu na chini. Hizo hali zinaeleweka na kutengana wazi. Huwa hazina katikati. Changamoto nyingi kwenye maisha yetu huwa zinatokana na kujaribu kukaa kati. Kushindwa kujitoa kweli kwenye upande mmoja wa kitu. (more…)

SheriaYaLeo (351/366); Kukikaribia kifo.

By | October 17, 2022

SheriaYaLeo (351/366); Kukikaribia kifo. Watu wengi huendesha maisha yao kwa mazoea na kupoteza muda kwenye mambo yasiyokuwa na tija. Ni mpaka pale wanapokutana na hatari ya kifo ndiyo wanayabadili maisha na kuishi kwa tija. Inaweza kuwa ni kwenye ajali ambayo mtu amenusurika kufa au kupata ugonjwa ambao hawezi kupona. Katika (more…)

2846; Cheza kamari kwako mwenyewe.

By | October 16, 2022

2846; Cheza kamari kwako mwenyewe. ‘Kila kitu kwenye maisha ni kamari….’ Ni kauli wanayopenda kuitumia wale wanaocheza kamari mbalimbali kwa kutegemea kupata matokeo makubwa bila kufanya kazi. Ni kweli kwamba kila kitu kwenye maisha ni kamari, kwa sababu hakuna kitu chochote ambacho kina uhakika wa asilimia 100. Kwa chochote tunachofanya (more…)