Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2901; Orodha na pesa.

By | December 10, 2022

2901; Orodha na pesa. Kwako rafiki yangu mpendwa unayekuwa ‘bize’ kila siku lakini huoni hatua kubwa ambazo unazipiga. Unakuwa ‘bize’ kweli kweli siku nzima, unakuwa huna muda kabisa. Lakini ukiangalia matokeo unayozalisha, hayaonekani kabisa. Kwa sehemu kubwa, wengi tumerithi mfumo wa kazi unaotumika kwenye ajira nyingi rasmi. Kwenye ajira hizo, (more…)

2900; Sikitika nao, lakini usinunue matatizo yao.

By | December 9, 2022

2900; Sikitika nao, lakini usinunue matatizo yao. Kwako rafiki yangu mpendwa ambaye unapojaribu kujenga urafiki na wateja, wao wanajaribu kuutumia kujinufaisha binafsi. Wanatumia fursa hiyo kukueleza matatizo yao binafsi na kutaka uwakopeshe kile unachouza. Kibinadamu, ni mambo ambayo yanaumiza na unashawishika kutaka kuwasaidia watu wa aina hiyo. Hapo ndipo ninapotaka (more…)

2899; Njia haipotezi.

By | December 8, 2022

2899; Njia haipotezi. Kwako rafiki yangu mpendwa ambaye umekuwa unajaribu njia mbalimbali lakini hupati matokeo unayotaka. Ni rahisi kujiambia tatizo lipo kwenye njia. Kwamba njia hiyo siyo sahihi na inapoteza. Lakini huo siyo ukweli, tatizo halipo kwenye njia, bali lipo kwenye namna unavyofanyia kazi njia hiyo. Kwa mfano, njia ya (more…)

2898; Muda upo.

By | December 7, 2022

2898; Muda upo. Kwako rafiki yangu mpendwa unayelalamika kwamba unachokosa ni muda ndiyo maana unashindwa kufanya yale unayopaswa kutafanya. Hii ni sababu au kisingizio ambacho kila mtu huwa anakitumia. Moja ya misingi yangu ni kwamba chochote kinachofanywa na wengi, hakiwezi kuwa sahihi kwako kupata matokeo bora. Hivyo basi, inapokuja kwenye (more…)

2897; Sababu hazitauza.

By | December 6, 2022

2897; Sababu hazitauza. Kwako rafiki yangu mpendwa unayeshangaa kwa nini unashindwa kuuza licha ya juhudi kubwa unazoweka. Kinachokuzuia kuuza ni sababu nyingi unazokuwa nazo juu ya yale unayofanya au kushindwa kufanya. Unashindwa kukaa kwenye mchakato na kutekeleza viwango ulivyojiwekea. Badala ya kukubali uvivu na uzembe uliopelekea hayo, wewe unajipa sababu (more…)

2896; Kupata viroboto.

By | December 5, 2022

2896; Kupata viroboto. Kwako rafiki yangu mpendwa unayeshangaa kwa nini mambo yako huwa yanakwama licha ya juhudi kubwa unazoweka. Ipo kauli inayosema; ukilala na mbwa utaamka na viroboto. Hii inamaanisha kwamba watu unaojihusisha nao huwa wanakuambukiza yale waliyonayo. Hivyo kama utajihusisha na watu walio hasi na ambao wamekata tamaa, wanaoahirisha (more…)

2895; Hakuna asiyefukuzika.

By | December 4, 2022

2895; Hakuna asiyefukuzika. Kwako rafiki yangu mpendwa ambaye umeshaliona tatizo kwenye biashara yako, lakini unashindwa kulitatua kwa sababu unaona kuna watu hawagusiki. Unaona ukiwagusa wale ambayo ndiyo chanzo cha matatizo ambayo biashara inayapitia, basi biashara itatikisika sana. Hilo linakufanya uendelee kukumbatia uvivu na uzembe unaokusumbua sana. Nina mambo machache ya (more…)

2894; Uko bize kufanya nini?

By | December 3, 2022

2894; Uko bize kufanya nini? Kwako rafiki yangu mpendwa ambaye kila wakati uko bize kiasi cha kukosa muda wa kuyafanyia kazi yake mapya unayojifunza. Pamoja na kuwa kwako bize, hakuna matokeo makubwa na ya tofauti unayozalisha. Na hapo ndipo swali langu linapokuja, uko bize kufanya nini? Kama mambo yanayokuweka bize (more…)

2893; Vinavyofundishika na visivyofundishika.

By | December 2, 2022

2893; Vinavyofundishika na visivyofundishika. Kwako rafiki yangu mpendwa ambaye unajaribu kuwafundisha wafanyakazi wako lakini hawafundishiki. Kuna vitu huwa vinafundishika kwa watu kirahisi na kuna vitu ambavyo havifundishiki kirahisi. Jinsi ya kuifanya kazi ni kitu ambacho kila mtu anaweza kufundishwa. Na kama ataweka umakini kwenye hilo, ataweza kuelewa na kufanya vizuri. (more…)

2892; Dikteta Mwema.

By | December 1, 2022

2892; Dikteta Mwema. Kwako rafiki yangu mpendwa ambaye umejaribu kuwapa wafanyakazi wako kile wanataka lakini bado hawakupi matokeo unayotaka. Wakati Elon Musk anainunua kampuni ya twitter, wengi hawakujua nini kinaenda kutokea. Waliona ni kama mzaha tu na kudhani hilo halitafanikiwa. Alipokamilisha manunuzi na kumfukuza mkurugenzi mkuu na yeye kushika nafasi (more…)