Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

2857; Tawala hisia zako.

By | October 27, 2022

2857; Tawala hisia zako. Sisi binadamu ni viumbe wa kihisia. Huwa tunafanya maamuzi yetu kwa hisia, kisha tunayahalisha kwa mantiki. Tatizo la hisia huwa hazina msimamo, ni kitu cha kupita kama mawimbi. Pia hisia zinaathiriwa na mambo mbalimbali. Ukiwa mtu unayetawaliwa na hisia, hutaweza kufanya chochote kikubwa kwenye maisha yako. (more…)

#SheriaYaLeo (360/366); Hili nalo litapita.

By | October 26, 2022

#SheriaYaLeo (360/366); Hili nalo litapita. Sisi binadamu huwa tunapenda sana uhakika wa mambo. Hilo ndiyo limekuwa linasababisha tukae kwenye mazoea. Huwa tunataka mambo na hali ziendelee kuwa vile ambavyo zimekuwa. Ndiyo maana mara nyingi huwa tunasema afadhali ya jana. Ukweli ni kwamba, kila kitu kinabadilika. Hakuna kitu chochote ambacho hakibadiliki (more…)

2856; Ishi kila siku kama ndiyo siku yako ya mwisho.

By | October 26, 2022

2856; Ishi kila siku kama ndiyo siku yako ya mwisho. Huwa tunaona tuna muda mwingi, mpaka pale tunapokuja kugundua muda wetu umeisha. Ni rahisi kujiambia utafanya kesho, kwa kuwa umezoea kuziona kesho nyingi. Lakini ipo siku ambayo hutaiona kesho uliyopanga. Ubaya ni huwezi kuijua siku hiyo ni ipi. Lakini uhakika (more…)

#SheriaYaLeo (359/366); Jiweke kwenye uwanja wa kifo.

By | October 25, 2022

#SheriaYaLeo (359/366); Jiweke kwenye uwanja wa kifo. Tangu enzi na enzi, majenerali wa majeshi wamekuwa wakitafuta njia ya kuwasukuma wanajeshi wao kupambana kwa kila namna ili kupata ushindi. Wapo ambao wamekuwa wakitunia maneno ya hamasa ili kuwahamasisha wanajeshi wao kupambana. Maneno hayo yamekuwa na mafanikio kiasi lakini nguvu yake huwa (more…)

2855; Wewe ni miujiza.

By | October 25, 2022

2855; Wewe ni miujiza. Kupatikana kwako ni tukio la miujiza mikubwa. Kukutana kwa wazazi wako, lilikuwa tukio ambalo hakuna aliyelitegemea. Wazazi wako kuamua kufanya mapenzi siku ambayo mimba yako ilitungwa pia ni tukio ambalo huenda lisingetokea. Kama mmoja wao angekuwa amesafiri au kuumwa, siku hiyo zoezi hilo lisingefanyika. Katika mbegu (more…)

#SheriaYaLeo (358/366); Epuka ukuaji wa kiroho feki.

By | October 24, 2022

#SheriaYaLeo (358/366); Epuka ukuaji wa kiroho feki. Changamoto kubwa tunayokabiliana nayo kwenye zama hizi ni wengi kushindwa kujua njia sahihi za ukuaji wa kiroho. Lengo la dini lilipaswa kuwa njia ya watu kupata ukuaji wa kiroho. Lakini kwa zama hizi, dini zimeshindwa kuwasaidia watu kwenye hilo. Badala yake zimewajaza hofu (more…)

2854; Ng’ang’ana mpaka ufanikiwe.

By | October 24, 2022

2854; Ng’ang’ana mpaka ufanikiwe. Wanaofanikiwa na wanaoshindwa wote huanza sawa. Huwa wanaanza na ndoto kubwa walizonazo. Kisha wanachukua hatua kwenye ndoto hizo. Katika kuchukua huko hatua huwa wanakutana na changamoto na vikwazo mbalimbali. Na hapa ndipo wanaofanikiwa na wanaoshindwa wanapotofautiana. Wanaoshindwa huwa wanakata tamaa haraka pale wanapokutana na vikwazo na (more…)

#SheriaYaLeo (357/366); Ujinga wa kiwango cha juu.

By | October 23, 2022

#SheriaYaLeo (357/366); Ujinga wa kiwango cha juu. Binadamu tunazaliwa, kuishi na kufa. Hivyo ndivyo maisha yamekuwepo tangu enzi na enzi na ndiyo imewezesha dunia kuendelea kuwepo. Viumbe wanaokufa wanatoa nafasi kwa wengine wanaozaliwa. Baadhi ya watu wanatafuta teknolojia ya kurefusha maisha au kuondoa kabisa kifo. Huu ni ujinga wa hali (more…)

2853; Ipokee kila siku kwa upendo.

By | October 23, 2022

2853; Ipokee kila siku kwa upendo. Upendo ndiyo nguvu kuu inayoiendesha dunia. Upendo ndiyo imani kuu inayowaleta watu wote pamoja. Upendo una nguvu kubwa ya kuleta mapinduzi kwenye maisha ya kila mtu. Ili kufanikiwa, unapaswa kuipokea kila siku kwa upendo mkuu. Unapaswa kuongozwa na upendo kila siku. Upendo unapaswa kuanzia (more…)

#SheriaYaLeo (356/366); Tumia kifo kuziondoa tofauti.

By | October 22, 2022

#SheriaYaLeo (356/366); Tumia kifo kuziondoa tofauti. Kifo ni moja ya vitu vinavyotuleta mahali pamoja wote. Ni kitu kinachotufanya wote kuwa sawa kwa sababu mwisho wa siku wote tutakufa. Haijalishi tofauti zetu kwenye maisha, wote njia yetu ni moja, kifo. Yote tunayobaguana nayo hayana tofauti kwenye kifo. Kwa kujua hatima hii (more…)