Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

SheriaYaLeo (351/366); Kukikaribia kifo.

By | October 17, 2022

SheriaYaLeo (351/366); Kukikaribia kifo. Watu wengi huendesha maisha yao kwa mazoea na kupoteza muda kwenye mambo yasiyokuwa na tija. Ni mpaka pale wanapokutana na hatari ya kifo ndiyo wanayabadili maisha na kuishi kwa tija. Inaweza kuwa ni kwenye ajali ambayo mtu amenusurika kufa au kupata ugonjwa ambao hawezi kupona. Katika (more…)

2846; Cheza kamari kwako mwenyewe.

By | October 16, 2022

2846; Cheza kamari kwako mwenyewe. ‘Kila kitu kwenye maisha ni kamari….’ Ni kauli wanayopenda kuitumia wale wanaocheza kamari mbalimbali kwa kutegemea kupata matokeo makubwa bila kufanya kazi. Ni kweli kwamba kila kitu kwenye maisha ni kamari, kwa sababu hakuna kitu chochote ambacho kina uhakika wa asilimia 100. Kwa chochote tunachofanya (more…)

#SheriaYaLeo (350/366); Kitambue kifo kwa vitendo.

By | October 16, 2022

#SheriaYaLeo (350/366); Kitambue kifo kwa vitendo. Huwa tunakihofia kifo kwa sababu tunajiweka mbali nacho. Imekuwa ikielezwa kwamba dawa ya hofu ni kufanya kile unachohofia. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye kifo, kama hutaki kukihofia, unapaswa kukitambua kifo kwa vitendo. Kujenga hali inayokukumbusha kifo kila wakati kiasi kwamba hukihofii tena. Moja ya (more…)

2845; Ni kufanya.

By | October 15, 2022

2845; Ni kufanya. Matokeo ni zao la kufanya. Haijalishi una mawazo na nia nzuri kiasi gani, kama hutafanya, hakuna matokeo utakayoyapata. Kuwa chanya au hasi haina maana kama hutafanya. Kipaumbele chako cha kwanza kinapaswa kuwa ni kufanya. Kufanya na kelele huwa haviendi pamoja. Wasiofanya watakuwa na maoni mengi kwako, jinsi (more…)

#SheriaYaLeo (349/366); Ondoka kwenye mazoea na kuiga.

By | October 15, 2022

#SheriaYaLeo (349/366); Ondoka kwenye mazoea na kuiga. Huwa tunaiangalia dunia kwa kutumia mazoea na kuiga wengine. Tunafanya yale tuliyozoea kufanya au tunayowaona wengine wakifanya. Kuna mengi ambayo tunashindwa kuyang’amua kutokana na mazoea tunayokuwa nayo. Hayo yanatutaka kwenda zaidi ya mazoea na kuiga. Yanatutaka tutumie uwezo mkubwa ulio ndani yetu kuweza (more…)

2844; Shtuka ni mtego.

By | October 14, 2022

2844; Shtuka ni mtego. Huwa kuna kichekesho kinasema ukiona choo kwenye ndoto usikitumie, ni mtego huo. Huenda unakumbuka hili vizuri utotoni, unaota unacheza, unaufurahia mchezo, halafu mkojo unakubana, unaenda kukojoa, unashtuka umekojoa kitandani. Kwenye maisha kuna mitego mingi inayowanasa watu kwa kukosa umakini wa kujua ni mitego. Moja wapo ni (more…)

#SheriaYaLeo (348/366); Jinsi ya kuiangalia dunia.

By | October 14, 2022

#SheriaYaLeo (348/366); Jinsi ya kuiangalia dunia. Watu wengi huwa wanaiangalia dunia kwa mazoea. Wanatumia yale waliyoyazoea kutafsiri yanayotokea na kufanya maamuzi. Wanapenda uhakika wa mazoea, hata kama hayaleti matokeo yaliyo bora. Wewe hupaswi kuwa hivyo, badala yake unapaswa kuiangalia dunia kama mchunguzi. Unapaswa kuiangalia dunia ukiwa tayari kujifunza na kujaribu (more…)

2843; Kuweka matumaini yako kwa wengine.

By | October 13, 2022

2843; Kuweka matumaini yako kwa wengine. Kuweka matumaini yako kwa wengine ndiyo kitu ambacho kimekuwa kinakuangusha kila mara. Huwa kuna usemi kwamba ndege anapotua kwenye tawi la mti, siyo kwa sababu anaamini tawi hilo ni imara, bali kwa sababu anaamini mabawa yake yanaweza kumrusha. Kama ndege angetua kwenye tawi kwa (more…)

#SheriaYaLeo (347/366); Maisha na kifo.

By | October 13, 2022

#SheriaYaLeo (347/366); Maisha na kifo. Tunaweza kuelezea tofauti kati ya maisha na kifo kwa namna ifuatayo; Kifo ni utulivu kamili, bila ya mwendo au mabadiliko, isipokuwa kuharibika. Kwenye kifo tunatenganishwa na wengine na kuwa wapweke. Kwa upande mwingine, maisha ni mwendo, muunganiko na viumbe wengine na utofauti wa maisha. Kwa (more…)

2842; Usitapeliwe tena.

By | October 12, 2022

2842; Usitapeliwe tena. Utapeli hautakuja kuisha duniani kwa sababu tatu; Moja, watu siyo waaminifu. Huwa wapo tayari kutumia njia yoyote hata isiyokuwa halali ili tu kupata wanachotaka. Mbili, watu hawapendi kufanya kazi. Hivyo hutafuta njia ya mkato ya kupata wanachotaka bila kuweka kazi. Tatu, watu wanapenda kufuata mkumbo. Wakiona wengi (more…)