Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (346/366); Mtazamo Wa Utoto.

By | October 12, 2022

#SheriaYaLeo (346/366); Mtazamo Wa Utoto. Kama tutakuwa wa kweli kuhusu maisha yetu, wengi wetu tutakubali kwamba hakuna jipya kwenye maisha yetu. Kila kitu kinaonekana cha kawaida na hakuna kinachotushangaza. Kuna kitu kikubwa tunajua kinakosekana kwenye maisha yetu, lakini ni vigumu kujua ni kipi hasa. Kujaribu kuondokana na hali hiyo, huwa (more…)

2841; Uchawi na ushirikina.

By | October 11, 2022

2841; Uchawi na ushirikina. Hadithi tulizokuwa tunajifunza utotoni zilikuwa na maana kubwa ambayo haikuwa rahisi kwa akili zetu za utoto kung’amua. Moja ya hadithi hizo ni SIZITAKI MBICHI HIZI. Kama unakumbuka, sungura aliona ndizi na kuzipenda. Akaanza kuzirukia, lakini hakuzifikia. Akaruka na kuruka tena, lakini wapi. Baada ya kuhangaika sana (more…)

#SheriaYaLeo (345/366); Ona kwa ujumla.

By | October 11, 2022

#SheriaYaLeo (345/366); Ona kwa ujumla. Sisi binadamu huwa tuna tabia ya kuona vitu kwa utengano. Tunajiona sisi na wengine kama watu binafsi na waliojitenga badala ya kujiona kama kitu kimoja ambacho kimeungana. Huwa tunaiangalia dunia kwa utengano wa viumbe na vitu mbalimbali, badala ya kuangalia jinsi vyote vinavyokuwa vimeungana pamoja. (more…)

2840; Hatupendi mambo magumu.

By | October 10, 2022

2840; Hatupendi mambo magumu. Kitu kimoja kuhusu sisi binadamu ni hiki, huwa hatupendi mambo magumu. Huwa tunapenda mambo rahisi kuyaelewa na kufanyia kazi. Na ndiyo maana matapeli huwa wana ushawishi mkubwa kwa watu. Kwa sababu huwa wanaelezea mambo kwa urahisi kabisa ambao mtu anaelewa. Ndiyo maana pia mambo yanayohusu burudani (more…)

#SheriaYaLeo (344/366); Vuka ubinadamu na fikia uwezo usio na ukomo.

By | October 10, 2022

#SheriaYaLeo (344/366); Vuka ubinadamu na fikia uwezo usio na ukomo. Mara nyingi tunaishi kwenye hali ya ubinadamu ambayo huwa ina ukomo mkubwa. Tunakuwa tumezama kwenye mazoea yetu ya kila siku, ambayo yanatuzuia kufikia uwezo usio na ukomo wa ulimwengu. Wapo wanaojaribu kuondoka kwenye hali hiyo, lakini bado hawafanikiwi kwa sababu (more…)

2839; Kukosa cha kufanya.

By | October 9, 2022

2839; Kukosa cha kufanya. Watu huwa wanapoteza muda kwa sababu wanakuwa hawana kitu kingine cha kufanya. Wengine wanatengeneza hata matatizo kwa sababu tu hawana cha kufanya. Kikubwa ambacho naendelea kujifunza kwenye maisha yetu wanadamu ni kwamba muda hauwezi kukaa mtupu, lazima kuna kitu kitajipenyeza tu. Hivyo basi, kama kweli unataka (more…)

#SheriaYaLeo (343/366); Ungana na kitu kikubwa kuliko wewe.

By | October 9, 2022

#SheriaYaLeo (343/366); Ungana na kitu kikubwa kuliko wewe. Mara nyingi changamoto tunazokutana nazo kwenye maisha huwa zinatupa msongo na hata sonona. Hilo huweza kututikisa kwa kiasi kikubwa na kutuzuia kufanya makubwa tunayotaka. Njia ya kuondoka kwenye hali hizo ni kuungana na kitu kikubwa kuliko wewe. Kwenye maisha yako kuna kipindi (more…)

2838; Ukishapotea, ni vigumu sana kurudi.

By | October 8, 2022

2838; Ukishapotea, ni vigumu sana kurudi. Kama umeshawahi kwenda mahali usipopajua kwa kufuata ramani ya kwenye simu (google map), unajua jinsi ambavyo unaweza kuwa unazunguka mahali pamoja kwa muda mrefu bila kujua. Hiyo ni kwa sababu ramani hizo zina udhaifu mmoja, kama imekuelekeza ukifika mbele kata kulia, halafu hukukata hapo (more…)

#SheriaYaLeo (342/366); Kutembea na kifo.

By | October 8, 2022

#SheriaYaLeo (342/366); Kutembea na kifo. Watu wengi huwa wanaishi maisha yasiyo na maana na kupoteza muda kwa kuona wana muda mwingi wa maisha. Ni mpaka pale wanapokutana na hali ya kukabiliana na kifo, ndipo wanaiona thamani ya muda na kuutumia kwa uangalifu mkubwa. Kwa mfano mtu anapogundulika kuwa na saratani (more…)

2837; Siyo kwa ajili yako, bali wao.

By | October 7, 2022

2837; Siyo kwa ajili yako, bali wao. Kitu kikubwa ninachoendelea kujifunza kwa kina kabisa kwenye safari ya mafanikio ni kwamba ili ufanikiwe, unapaswa kwenda kinyume kabisa na tabia zetu za asili kama binadamu. Tabia kama uvivu, wivu, chuki, ubinafsi na nyingine, ni sehemu ya asili yetu binadamu. Lakini ukiziendekeza hizo, (more…)