Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (341/366); Muda hai au muda mfu?

By | October 7, 2022

#SheriaYaLeo (341/366); Muda hai au muda mfu? Muda ambao upo hai ndiyo kitu pekee unachokimiliki. Vitu vingine vyote ulivyonavyo unaweza kuvipoteza – familia yako, nyumba, magari, kazi na hata biashara. Muda ambao upo hai ndiyo kitu pekee kilicho ndani ya udhibiti wako. Jinsi ya kutumia muda wako, ni maamuzi yako (more…)

2836; Udhaifu ndiyo uimara.

By | October 6, 2022

2836; Udhaifu ndiyo uimara. Kwa maisha yetu yote tumekuwa tukidanganywa. Tumekuwa tunaambiwa tuyafanyie kazi madhaifu yetu kwa kuyaondoa ili tuwe imara. Hilo linafanyika kwa nia nzuri, ila matokeo yake huwa siyo mazuri. Pale mtu anapohangaika kuondoa madhaifu yake na kuyageuza kuwa uimara, kinachotokea ni madhaifu hayo yanakuwa makubwa na yenye (more…)

#SheriaYaLeo (340/366); Zamisha akili yako kwenye wakati uliopo.

By | October 6, 2022

#SheriaYaLeo (340/366); Zamisha akili yako kwenye wakati uliopo. Kutokutulia kwa akili zetu imekuwa ndiyo chanzo kikubwa cha kukosa umakini na kufanya makosa ambayo yanatugharimu sana. Kwa asili, akili yetu haiwezi kutulia sehemu moja, huwa inahama kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine. Akili zetu ni rahisi sana kuhamishwa na usumbufu unaokuwa (more…)

2835; TUTATUA TATIZO HILI KWANZA.

By | October 5, 2022

2835; TUTATUA TATIZO HILI KWANZA. ASILIMIA 90 YA MATATIZO ULIYONAYO, YANAWEZA KUTATULIWA NA FEDHA. NA HIYO ASILIMIA 10 AMBAYO HAIWEZI KUTATULIWA NA FEDHA, HUNA CHA KUFANYA. KWA HIYO BASI, TATIZO LAKO KUBWA SIYO MATATIZO ULIYONAYO, BALI NI FEDHA. HIVYO UNA TATIZO MOJA KUBWA LA KUTATUA MBELE YAKO, FEDHA. KAMA BADO (more…)

#SheriaYaLeo (339/366); Ulimwengu upo ndani yako.

By | October 5, 2022

#SheriaYaLeo (339/366); Ulimwengu upo ndani yako. Kama unataka kuelewa ukubwa na ukuu wa ulimwengu usio na ukomo, anza kwa kuangalia ubongo wako. Ndani ya ubongo wako kuna miunganiko ya seli zaidi ya milioni bilioni moja. Kama ingebidi uhesabu miunganiko hiyo, mmoja kwa kila sekunde, ingekuchukua miaka milioni 32 kukamilisha. Ukiangalia (more…)

2834; Mwache akuambie mwenyewe.

By | October 4, 2022

2834; Mwache akuambie mwenyewe. Huwa tunajikatalia mambo mengi sisi wenyewe kuliko tunavyokataliwa na wengine. Ninachoweza kusema kwa uhakika ni kwamba yale hapana za watu ambazo umekuwa unajipa wewe mwenyewe ni nyingi kuliko hapana unazosikia kweli kutoka kwa watu. Yaani majibu unayojipa kwamba watu watakataa kitu fulani kama utawaambia ni mengi (more…)

#SheriaYaLeo (338/366); Kiangalie kifo chako.

By | October 4, 2022

#SheriaYaLeo (338/366); Kiangalie kifo chako. Wengi wetu huwa tunatumia muda mwingi wa maisha yetu kujaribu kukiepuka kifo. Kifo ni kitu ambacho hakuna namna tunaweza kukikwepa, hivyo tunapaswa kukifikiria muda wote. Kwa kuelewa ufupi wa maisha yetu hapa duniani, inatufanya tuishi kwa kusudi na kuyaharakishia malengo yetu. Kujifunza kukubaliana na uhalisia (more…)

#SheriaYaLeo (337/366); Tukio ambalo huenda lisingetokea.

By | October 3, 2022

#SheriaYaLeo (337/366); Tukio ambalo huenda lisingetokea. Huwa tunayachukulia maisha kikawaida na kwa mazoea. Lakini tukitafakari kwa kina, ni tukio ambalo huenda lisingetokea. Tangu kuanza kwa maisha hapa duniani, mabilioni ya miaka iliyopita, kila tukio limekuwa linatokea kwa namna ambayo haiwezi kuelezeka. Hata wakati sisi binadamu tunajitenga na wanyama wengine na (more…)

2832; Gharama ya kuepuka watu wa kawaida.

By | October 2, 2022

2832; Gharama ya kuepuka watu wa kawaida. Ili ufanikiwe, unawahitaji sana watu. Lakini watu hawalingani. Kuna watu wa kawaida, ambao ndiyo wengi. Hawa pia ni rahisi kuwapata. Halafu kuna watu wasio wa kawaida, ambao ni wachache na wagumu kuwapata. Ili upate mafanikio makubwa, unahitaji kuwaepuka watu wa kawaida na kuwapata (more…)