Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (336/366); Ulimwengu wa kushangaza na usio na ukomo.

By | October 2, 2022

#SheriaYaLeo (336/366); Ulimwengu wa kushangaza na usio na ukomo. Ulimwengu ni wa kushangaza na usio na ukomo. Katika kulielewa na kulisimamia hilo, jamii mbalimbali zimekuwa na tararibu zake. Ni taratibu ambazo zinalenga kuwafanya watu waweze kuyathamini maisha yao hapa duniani. Matambiko, ubatizo na hata taratibu nyingine za kimila, kifalsafa na (more…)

2831; Foleni ya kushangaa.

By | October 1, 2022

2831; Foleni ya kushangaa. Siku iliyopita nikiwa barabarani nilikutana na foleni ndefu, ambayo ilituchukua muda. Kwa kuwa halikuwa eneo lililozoeleka kuwa na foleni, nilijiambia patakuwa na ajali mbele ambayo imeziba barabara. Foleni ikasogea, tulipofika sehemu inayosababisha foleni sikuamini macho yangu. Barabara ilikuwa nyeupe kabisa, ila kuna gari ilikuwa imeacha barabara (more…)

#SheriaYaLeo (335/366); Nenda mbele kwa kusudi.

By | October 1, 2022

#SheriaYaLeo (335/366); Nenda mbele kwa kusudi. Kwenye historia ya jeshi, kuna aina mbili za majeshi. Aina ya kwanza ni jeshi linalopigana kwa kusudi kubwa. Jeshi hilo huwa tayari kupambana kwa kila aina na hata kufia katika mapambano. Aina ya pili ni jeshi linalopigana kama sehemu ya kazi na kupata pesa. (more…)

2830; Matokeo hayadanganyi.

By | September 30, 2022

2830; Matokeo hayadanganyi. Nimewahi kushirikisha huu mfano, ila nitaurudia tena kwa msisitizo zaidi. Wakati tupo sekondari, mwalimu wetu wa hesabu alikuwa anasahihisha mitihani kwenye majibu tu. Hakuwa anajisumbua kuangalia njia. Wanafunzi tukajadiliana na kuona hilo halipo sawa, hivyo tukamwuliza mwalimu kwa nini hasahihishi njia? Maana anatunyima maksi kwenye njia. Mwalimu (more…)

#SheriaYaLeo (334/366); Mwendeshaji na farasi.

By | September 30, 2022

#SheriaYaLeo (334/366); Mwendeshaji na farasi. Uhusiano kati ya fikra na hisia zetu ni kama mwendesha farasi na farasi. Hisia zetu ni farasi na fikra zetu ni mwendesha farasi. Farasi ana nguvu kubwa, lakini bila ya kuongozwa vyema anaishia kuzunguka huku na huko na kutokuleta matokeo yoyote yenye tija. Hivyo ndivyo (more…)

2829; Kuwaona huruma wasiojionea huruma.

By | September 29, 2022

2829; Kuwaona huruma wasiojionea huruma. Changamoto zetu kubwa kwenye maisha zinatokana na watu. Ni changamoto kubwa kwa sababu tunawahitaji sana watu, lakini ndiyo hivyo wanakuja na mambo yao ambayo yanatupa changamoto. Kwa kuwa tunawahitaji sana watu, kuna wakati tunakuwa hatutaki kuwapoteza, hivyo licha ya chagamoto wanazosababisha, tunaendelea kuwa nao. Na (more…)

#SheriaYaLeo (333/366); Jifunze kwenye zama zilizopita.

By | September 29, 2022

#SheriaYaLeo (333/366); Jifunze kwenye zama zilizopita. Vile tunavyoishi sasa ni matokeo ya mambo yaliyotokea kipindi cha nyuma. Mabadiliko yote ambayo binadamu tumeyapitia tangu enzi na enzi, ndiyo yamezalisha yote tuliyonayo sasa. Huwa tuna tabia ya kubeza zama zilizopita, kwa kuona zimepitwa na wakati. Kufanya hivyo kunatuzuia tusijifunze. Lakini pia ni (more…)

2828; Mteja mpya rahisi kumpata.

By | September 28, 2022

2828; Mteja mpya rahisi kumpata. Hakuna kitu kigumu kwenye biashara kama kupata mteja mpya. Kutokana na kudanganywa na kuumizwa kwa muda mrefu, wateja wana wasiwasi sana na biashara mpya kwao. Ahadi nyingi unazowapa wanakuwa hawana uhakika kama kweli zitatimia. Hilo ndiyo limekuwa linasababisha wasiwe tayari kununua, licha ya kuwa kuwapa (more…)

#SheriaYaLeo (332/366); Huwajui watu kama unavyodhani unawajua.

By | September 28, 2022

#SheriaYaLeo (332/366); Huwajui watu kama unavyodhani unawajua. Hatari kubwa uliyonayo ni kudhani unaweza kuwajua na kuwaelewa vizuri watu kwa mwonekano wa haraka wa nje. Watu wanaokuzunguka wamevaa sura ya kuigiza mbele yako, wakitaka waonekane kwa namna fulani, ambayo ni tofauti na uhalisia wao. Kama utakuwa haraka kukimbilia kuamua, utaishia kuamua (more…)

2827; Ung’ang’anizi na upinzani.

By | September 27, 2022

2827; Ung’ang’anizi na upinzani. Hakuna chochote unachokitaka kwenye maisha yako ambacho utakipata kwa urahisi. Chochote kile unachokitaka, dunia itakuwekea upinzani mkali kwenye kukipata. Dunia itahakikisha inakuwekea kila aina ya kikwazo, mradi tu usipate unachotaka. Njia pekee ya kuvuka upinzani wa dunia ni kuwa na ung’ang’anizi usiokuwa na kikomo. Unapaswa kuwa (more…)