Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (326/366); Ungana na kilicho karibu yako.

By | September 22, 2022

#SheriaYaLeo (326/366); Ungana na kilicho karibu yako. Maisha ni mafupi na nguvu zetu zina ukomo. Kwa kuongozwa na tamaa zetu, tunaweza kupoteza muda na nguvu kwenye kutafuta mabadiliko. Kwa ujumla, hupaswi kusubiri na kutumaini mambo yatakwenda vizuri, bali unapaswa kutumia vizuri kile ulichonacho. Asili inakuunga mkono. Kwa kuzamisha akili yako (more…)

2821; Kila mtu anafanya.

By | September 21, 2022

2821; Kila mtu anafanya. Sababu ya hovyo kabisa ya kufanya kitu ni kila mtu kuwa anakifanya. Sisi binadamu kama viumbe wa kimamii huwa tunapenda sana kufuata mkumbo. Lakini tuanze tu kwa kuuangalia ukweli ulivyo. Watu wengi kwenye jamii hawafanikiwi. Kwa kuwa wale tunaojihusisha nao wana ushawishi mkubwa kwetu, tunapaswa kuwaepuka (more…)

#SheriaYaLeo (325/366); Fokasi na vipaumbele.

By | September 21, 2022

#SheriaYaLeo (325/366); Fokasi na vipaumbele. Baadhi ya mambo unayofanya ni upotevu wa muda wako. Baadhi ya watu unaojihusisha nao ni wa hadhi ya chini, ambao watakuvuta urudi chini. Unapaswa kuepuka mambo na watu hao kama ukoma ili kutumia muda wako vizuri. Macho yako yanapaswa kuwa kwenye malengo yako makuu na (more…)

#SheriaYaLeo (324/366); Hatima ya maisha yako.

By | September 20, 2022

#SheriaYaLeo (324/366); Hatima ya maisha yako. Watu wote waliowahi kufanya makubwa hapa duniani walikuwa ni watu wa kuamini maisha yao yana hatima kubwa. Hawakukubali kuyumbishwa kwa namna yoyote ile kwenye hilo. Waliamini wanakwenda kufanya makubwa mpaka jamii iliyowazunguka nayo ikawaamini kwenye hayo. Kwa imani hiyo isiyoyumbishwa, waliweza kufanya makubwa sana. (more…)

2819; Umechagua mwenyewe.

By | September 19, 2022

2819; Umechagua mwenyewe. Hakuna jambo linaloshangaza kwenye maisha kama hili, watu kulalamikia na kulaumu wengine kwa machaguo yao wenyewe. Kwa zama tunazoishi sasa, hakuna yeyote anayekulazimisha kufanya chochote. Ni wewe mwenyewe umechagua. Chukua mfano wa mtu anayefanya kazi na analipwa mshahara kidogo. Anaweza kumlaumu mwajiri wake kwa kutokumjali, lakini hayo (more…)

#SheriaYaLeo (323/366); Angalia nje yako pia.

By | September 19, 2022

#SheriaYaLeo (323/366); Angalia nje yako pia. Kwa asili sisi binadamu huwa tunajiangalia sisi wenyewe zaidi. Huwa tunajali zaidi kuhusu changamoto zetu na matakwa yetu pia. Wewe unapaswa kwenda kinyume na hili kadiri iwezekanavyo. Na utaweza kulifanya hilo kwa njia tatu; Kwanza unakuwa msikilizaji makini. Unaweka umakini wako wote kwa wengine, (more…)

2818; Mwenza, roho mbaya au utegemezi.

By | September 18, 2022

2818; Mwenza, roho mbaya au utegemezi. Kuanzisha biashara na kuikuza mpaka ifikie mafanikio makubwa ni kitu kigumu sana kufanya, lakini ambacho kinawezekana kwa uhakika. Hatari kubwa na ya kwanza kwenye biashara ni kufa. Takwimu zinaonyesha biashara nyingi sana huwa zinakufa kwenye hatua ya uchanga. Zaidi ya asilimia 80 ya biashara (more…)

#SheriaYaLeo (322/366); Linganisha ubunifu na uhalisia.

By | September 18, 2022

#SheriaYaLeo (322/366); Linganisha ubunifu na uhalisia. Chochote unachofanya, huwa kinaanza na mawazo yako ya kibunifu. Kadiri unavyokwenda unakazana kuwa na ubunifu zaidi ili kufanya kitu cha tofauti. Unapoanza kufanya kulingana na mawazo yako ya kibunifu, kuna matokeo unayoyapata na mrejesho kutoka kwa wengine. Hapa unahitaji sana kupata maoni ya wengine (more…)

2817; Uwajibikaji na Mchakato.

By | September 17, 2022

2817; Uwajibikaji na Mchakato. Unataka kufanikiwa? 1. Jua unachotaka. 2. Panga jinsi ya kukipata. 3. Chukua hatua. 4. Kaa kwenye mchakato. 5. Wajibika. Unaanza kwa kujua nini unachotaka kwa uhakika kabisa. Mafanikio kwako yana maana gani? Hili lazima lianzie ndani yako, kwa kujisikiliza wewe mwenyewe. Unaweza kushangaa, lakini ukweli ni (more…)