Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (321/366); Tumia kivuli chako.

By | September 17, 2022

#SheriaYaLeo (321/366); Tumia kivuli chako. Tumeshaona jinsi ambavyo kila mtu ana kivuli ndani yako. Sehemu ya nafsi ya mtu ambayo anapenda kuificha kwa sababu haikubaliki sana kwa wengine. Nafsi hiyo huwa inakuwa na nguvu kubwa kama itaweza kutumiwa vizuri. Hivyo wajibu wako ni kuangalia namna gani unavyoweza kutumia kivuli chako (more…)

2816; Kuhimili mikiki mikiki.

By | September 16, 2022

2816; Kuhimili mikiki mikiki. Huwa kuna kichekesho ambapo mtu anasema kila akipata ufunguo wa mafanikio, anakuta kitasa kimebadilishwa. Hivyo inabidi aanze kutafuta tena ufunguo mwingine. Na akiupata tu, vitasa vinabadilishwa tena. Sijui kama umeipata picha hapo, maana huo ndiyo uhalisia kamili wa maisha yetu. Tunaweza kupambana sana ili kupata kitu (more…)

#SheriaYaLeo (320/366); Kuwa na roho ya ukarimu.

By | September 16, 2022

#SheriaYaLeo (320/366); Kuwa na roho ya ukarimu. Wote tumebeba majeraha na maumivu mbalimbali tangu utotoni. Kwenye maisha yetu ya kijamii, kadiri tunavyokua, tunakutana na hali za kuangushwa na kukatishwa tamaa. Hali hizo hutufanya tujione hatuna thamani na wala hatustahili vitu vizuri kwenye maisha. Wote huwa tuna nyakati za wasiwasi juu (more…)

#SheriaYaLeo (319/366); Igiza chenye ushawishi.

By | September 15, 2022

#SheriaYaLeo (319/366); Igiza chenye ushawishi. Katika nyakati zozote tunazoishi, huwa kuna tabia fulani ambazo huwa zinaonekana chanya na kukubalika na wengine. Hizo ndizo tabia unazopaswa kujua jinsi ya kuzionyesha ili ukubalike na wengine na uwe na ushawishi. Kwa mfano, kuonekana mtakatifu kwa nje ni kitu ambacho hakijawahi kupitwa na wakati. (more…)

2814; Acha kujikwamisha.

By | September 14, 2022

2814; Acha kujikwamisha. Ni jambo la kushangaza, lakini ndivyo uhalisia ulivyo, umekuwa unajikwamisha sana wewe mwenyewe. Pale mambo yanapokwenda vizuri kabisa kwa upande wako, unayaingilia na kuyavuruga. Unaharibu kile ambacho tayari kilishakuwa cha uhakika kwa kushindwa tu kuwa na utulivu na msimamo. Kutaka kwako vitu vipya na vinavyosisimua kunakufanya uharibu (more…)

#SheriaYaLeo (318/366); Usivurugwe na wapumbavu.

By | September 14, 2022

#SheriaYaLeo (318/366); Usivurugwe na wapumbavu. Huwezi kuwa kila mahali na huwezi kupambana na kila mtu. Muda wako na nguvu zako ni rasilimali zenye uhaba, unapaswa kujifunza jinsi ya kutunza rasilimali hizo. Kuchoka na kuvurugwa ni matokeo ya upotevu wa rasilimali hizo na inavuruga sana uwepo wa kiakili. Dunia imejaa wapumbavu (more…)

2813; Kwanza umefanya?

By | September 13, 2022

2813; Kwanza umefanya? Huwa ni rahisi kuyaangalia matokeo na kukatishwa nayo tamaa pale yanapokuwa tofauti na mategemeo. Lakini mtu unasahau kwamba matokeo yoyote yale huwa hayaji kimiujiza. Bali yanaathiriwa na kile ambacho mtu amefanya. Hivyo kabla hujaumizwa na matokeo, kwanza jiulize umefanya? Je umefanya kile unachopaswa kufanya? Kama jibu ni (more…)

#SheriaYaLeo (317/366); Vunja agano la mazoea.

By | September 13, 2022

#SheriaYaLeo (317/366); Vunja agano la mazoea. Kuna mazoea ambayo tayari yameshajengeka na yanazingatiwa sana kwenye jamii. Jinsi watu wanavyopaswa kuwa, vitu wanavyopaswa kusema na kufanya tayari vimeainishwa. Hali hizo zinakuwa zimejengwa kwenye tofauti za kijinsia, kikabila, kielimu na nyinginezo. Kukaa kwenye maagano haya ya mazoea ni kujizuia usifanye makubwa, kwani (more…)

2812; Kwanza umefanya?

By | September 12, 2022

2812; Kwanza umefanya? Hakuna kitu kinashangaza kama pale mtu anajua anachopaswa kufanya, ila hakifanyi, halafu analalamika kwa kukosa matokeo aliyotegemea. Hakuna namna matokeo yoyote yatakuja kimiujiza kwako bila ya kuchukua hatua na kufanya. Ukiangalia kila matokeo ambayo unayapata kwenye maisha yako, yanaendana kabisa na hatua ambazo ulichukua huko nyuma. Kama (more…)