Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (276/366); Hakuna chenye nguvu kuzidi asili ya mwanadamu.

By | August 3, 2022

#SheriaYaLeo (276/366); Hakuna chenye nguvu kuzidi asili ya mwanadamu. Watu wengi hudhani ujuzi wa asili ya binadamu umepitwa na wakati. Huona kwa maendeleo ya teknolojia tuliyonayo, tunepiga hatua kuondoka kwenye asili yetu binadamu na kuwa bora zaidi. Lakini hilo siyo kweli. Pamoja na mabadiliko makubwa ambayo yameendelea kwenye kila eneo (more…)

#SheriaYaLeo (275/366); Sheria ya msingi ya asili ya binadamu.

By | August 2, 2022

#SheriaYaLeo (275/366); Sheria ya msingi ya asili ya binadamu. Sisi binadamu wote huwa tuna asili ya aina moja. Kwa ujumla sisi binadamu wote ni viumbe wa kihisia, ambao huwa tunafanya maamuzi yetu kwa kusukumwa na hisia. Lakini sheria ya msingi kabisa ya asili ya binadamu imekuwa ni kukataa asili yake. (more…)

2770; Lazima uwaamini watu.

By | August 1, 2022

2770; Lazima uwaamini watu. Jamii zote zimejengwa kwenye msingi wa kuaminiana. Ni pale watu wanapoaminiana ndiyo jamii inakuwa imara na watu kufanikiwa. Na pale imani baina ya watu inapokosekana, jamii inakuwa dhaifu na watu kushindwa. Ni imani kwa wengine kwamba wanajua wanachofanya na wana nia njema ndiyo inafanya kila jamii (more…)

#SheriaYaLeo (274/366); Usiende zaidi ya lengo.

By | August 1, 2022

#SheriaYaLeo (274/366); Usiende zaidi ya lengo. Kiini cha mkakati ni kudhibiti kile kinachofuata baada ya kufikia lengo. Maana ushindi huwa una hatari ya kuvuruga kile kinachofuata kwa njia mbili. Moja ni kutaka kurudia kufanya yale uliyofanya ukidhani yatakupa matokeo uliyopata. Unajikuta ukijenga mazoea bila hata kuangalia kama ni mazoea sahihi (more…)

2769; Mtego wa mafanikio.

By | July 31, 2022

2769; Mtego wa mafanikio. Watu wengi huwa wanashangazwa na hili; kuna watu wanaanzia chini kabisa, wanapambana kweli kweli na kuyapata mafanikio makubwa, kisha wanaanguka. Hilo limekuwa linaonekana kwa wengi wanaoanzia chini, kupanda juu, kisha kushuka tena chini. Hali hiyo imekuwa ikisababishwa na mtego wa mafanikio ambao wengi wamekuwa hawauelewi. Mtego (more…)

#SheriaYaLeo (273/366); Kuwa tayari kubadilika.

By | July 31, 2022

#SheriaYaLeo (273/366); Kuwa tayari kubadilika. Kila kitu kwenye maisha huwa kinabadilika. Hivyo unapaswa kuchukulia kila kitu kwa kuendana na hali uliyonayo. Maji ndiyo kitu chenye nguvu zaidi duniani, kwa sababu huwa yapo tayari kubadilika. Maji huchukua nafasi kwenye chombo chochote ambacho yanawekwa. Hivyo kuwa tayari kubadilika kama maji ndiyo mkakati (more…)

#SheriaYaLeo (272/366); Pangilia mpaka mwisho.

By | July 30, 2022

#SheriaYaLeo (272/366); Pangilia mpaka mwisho. Hatari nyingi kwenye maisha, ambazo zipo mbele yetu, huwa zinaweza kuepukika kama tukiwa na mipango mizuri mpaka mwisho. Mara nyingi huwa tunachukua hatua ya kutatua tatizo dogo, lakini tunaishia kuzalisha tatizo kubwa zaidi. Kwenye mamlaka, nguvu kubwa ipo kwenye vitu unavyoacha kufanya kuliko vile unavyovifanya. (more…)

2767; Wanaheshimu unachokagua.

By | July 29, 2022

2767; Wanaheshimu unachokagua. Umewahi kukubaliana kitu na mtu, kuhusu mambo anayopaswa kubadili. Anakubali kabisa na anaanza kubadilika. Lakini baada ya muda mfupi anarudi kule kule alikotoka. Anayaacha mabadiliko na kurudi kwenye mazoea. Unaweza kushangazwa na kuumizwa na hali ya aina hiyo. Iweje mtu akubali kitu halafu baadaye abadilike? Ambacho huelewi (more…)