Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (256/366); Muda ndiyo kitu pekee ulichonacho.

By | July 14, 2022

#SheriaYaLeo (256/366); Muda ndiyo kitu pekee ulichonacho. Muda ni rasilimali muhimu sana uliyonayo kwenye maisha yako. Kuweza kutumia muda wako vizuri kunakufanya uweze kufanya makubwa zaidi. Ili kuweza kunufaika vizuri na muda, lazima uuchukulie kwa tofauti na ambavyo umekuwa unauchukulia. Kiuhalisia, tangu siku uliyozaliwa, muda ndiyo kitu pekee ulichonacho. Ndiyo (more…)

2751; Kujua, kuweza na kufanya.

By | July 13, 2022

2751; Kujua, kuweza na kufanya. Kama leo hii, utaacha kabisa kujifunza vitu vipya, yaani usijifunze chochote kipya, ila ukafanyia kazi yale ambayo tayari unayajua, bado utapata mafanikio makubwa sana. Kwa mfano ukaweka juhudi kubwa kwenye kazi/biashara yako kila mara. Ukawa na matumizi madogo kuliko kipato chako na hivyo kuweka akiba (more…)

#SheriaYaLeo (255/366); Imani ya shujaa.

By | July 13, 2022

#SheriaYaLeo (255/366); Imani ya shujaa. Asili huwa inaweka ukomo kwa kila kiumbe hai, ukomo wa mwisho ukiwa ni kifo. Huwa tuna ukomo kwenye kiasi cha nguvu tunachoweza kutumia kabla hatujachoka. Kadhalika kwenye muda na vipaji, tunavyo ila kwa ukomo mkubwa. Samaki hawezi kuruka angali na wala ndege hawezi kuishi ndani (more…)

2750; Siyo pale unapojisikia.

By | July 12, 2022

2750; Siyo pale unapojisikia. Huwezi kufanikiwa kama unafanya vitu pale unapojisikia kufanya. Mafanikio yanataka nidhamu kubwa sana ya kupanga na kufanya iwe unajisikia au la. Na hiyo ndiyo tofauti kuu kati ya wanaofanikiwa na wanaoshindwa. Wote wanakuwa na ndoto kubwa. Na wote wanaweka mipango ya kufikia ndoto hizo. Ila tofauti (more…)

#SheriaYaLeo (254/366); Puuza mambo kuyanyima nguvu.

By | July 12, 2022

#SheriaYaLeo (254/366); Puuza mambo kuyanyima nguvu. Jambo lolote lile huwa linakuwa na nguvu kwetu pale tunapolijali na kulipa umakini wetu. Hata watu huwa wanatusumbua kwenye mambo ambayo tunayajali sana. Lakini unapopuuza jambo lolote lile, unalinyima nguvu na hivyo halikusumbui. Hata watu wanapotaka kukusumbua, ukiwapuuza usumbufu wao unakosa nguvu kwako. Kupuuza (more…)

2749; Kama inabidi ulazimishwe, kuna tatizo.

By | July 11, 2022

2749; Kama inabidi ulazimishwe, kuna tatizo. Siku za karibuni nilikuwa naangalia mahojiano ya aliyekuwa mchezaji bora kabisa wa mpira wa kikapu Kobe Brayant. Aliulizwa yeye kama kiongozi alikuwa anawasukumaje wachezaji wenzake ili waweze kufanya vizuri kama timu. Jibu ambalo Kobe alitoa lilinifikirisha sana na nikaona siyo tu kwenye michezo, bali (more…)

#SheriaYaLeo (253/366); Ona hatari kubwa iliyo mbele yako.

By | July 11, 2022

#SheriaYaLeo (253/366); Ona hatari kubwa iliyo mbele yako. Changamoto kubwa ambayo watu wengi wanayo ni kunasa kwenye wakati uliopo na kushindwa kabisa kupangilia yale yanayokuja. Matokeo yake ni mambo yanakuja kwao kwa mshangao mkubwa, wakiwa hawana maandalizi yoyote, kitu ambacho kinawaathiri sana. Wewe usiwe kama walio wengi, usikubali kuvurugwa na (more…)

#SheriaYaLeo (252/366); Tumia vizuri machafuko.

By | July 10, 2022

#SheriaYaLeo (252/366); Tumia vizuri machafuko. Fikiria akili yako kama jeshi. Jeshi linapaswa kuweza kuendana na ugumu na machafuko yanayoendelea kwa kutumia njia isiyotabirika. Kama ilivyo kwenye vita vya msitumi, adui hatumii mkakati wote mazoea, badala yake kila wakati anakuwa kwenye mwendo. Hali hiyo inafanya kuwa vigumu sana kumshambulia adui huyo. (more…)