Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (261/366); Linganisha matokeo na njia.

By | July 19, 2022

#SheriaYaLeo (261/366); Linganisha matokeo na njia. Majenerali wote bora huwa wanaanza kwa kuangalia njia walizonazo kisha kutengeneza mkakati wa kuweza kuzitumia vyema ili kupata matokeo wanayoyataka. Wanaanza kwa kufikiria uhalisia ulivyo, kwa upande wao na wa maadui pamoja na mambo mengine yote yanauohusika kwenye mapambano. Kufanya hivyo kunawapa msingi sahihi (more…)

2756; Unakulaje chakula kitamu?

By | July 18, 2022

2756; Unakulaje chakula kitamu? Rafiki, kipi huwa ni chakula kitamu kwako na unachokipenda sana? Je wakati wa kula chakula hicho huwa unaharakisha ukimalize haraka? Upi ni mchezo au burudani unayopenda kufuatilia sana? Je wakati unafuatilia mchezo au burudani hiyo huwa unataka kuharakisha ili kumaliza haraka? Na je ni watu gani (more…)

#SheriaYaLeo (260/366); Waondoe kwenye upande hasi.

By | July 18, 2022

#SheriaYaLeo (260/366); Waondoe kwenye upande hasi. Ni rahisi kukaa upande hasi kuliko upande chanya. Ni rahisi kukosoa watu kuliko kuwasifia. Ndiyo maana watu wengi huwa wanakimbilia kwenye huo upande hasi. Inahitaji jitihada kubwa kukaa upande chanya na kueleza ubora wa kitu. Ni rahisi kukaa upande hasi na kuonyesha udhaifu wa (more…)

2755; Unakimbilia wapi?

By | July 17, 2022

2755; Unakimbilia wapi? Hebu pata picha unapita njiani na kukutana na mtu unayemfahamu, anatembea kwa haraka sana. Unamsimamisha ili kumsalimia anakujibu kwa haraka na kuendelea na kasi yako, anakuambia anataka kuwahi. Unamuuliza kwani unawahi wapi? Anakujibu hata sijui, ila nataka tu kuwahi. Je utamwelewaje mtu wa aina hii? Ni dhahiri (more…)

#SheriaYaLeo (259/366); Achana na mazoea.

By | July 17, 2022

#SheriaYaLeo (259/366); Achana na mazoea. Majenerali bora wa kivita na wanamikakati wabunifu huwa wanafanikiwa siyo kwa sababu ya ujuzi walionao, ila kwa sababu wanaweza kuachana na mazoea na kuweka umakini wao kwenye wakati uliopo. Hivyo ndivyo ubunifu unavyochochewa na fursa kutumiwa. Maarifa, ujuzi na uzoefu huwa vina ukomo. Hakuna kiwango (more…)

2754; Muda wa kazi na muda unaofanya kazi.

By | July 16, 2022

2754; Muda wa kazi na muda unaofanya kazi. Hakuna eneo ambalo watu wengi huwa wanajidanganya kama kwenye muda. Na usipokuwa mkweli kwenye muda wako mwenyewe, hakuna namna unaweza kufanikiwa. Watu wawili, wanaweza kufanya kitu cha aina moja na kuonekana wakiwa na muda unaolingana. Bado mmoja akafanikiwa zaidi ya mwingine. Tofauti (more…)

#SheriaYaLeo (258/366); Usitaharuki.

By | July 16, 2022

#SheriaYaLeo (258/366); Usitaharuki. Huwa ni kawaida yetu sisi binadamu kutaharuki pale tunapokutana na mambo makubwa na ya tofauti na tulivyozoea. Lakini kutaharuki huko huwa hakuna msaada wowote, zaidi ya kutufanya tuwe dhaifu zaidi na kuwa kwenye hali ya kushindwa. Jambo lolote linalotokea, hata liwe kubwa na la tofauti kiasi gani, (more…)

#SheriaYaLeo (257/366); Fikiria matokeo yasiyotegemewa.

By | July 15, 2022

#SheriaYaLeo (257/366); Fikiria matokeo yasiyotegemewa. Sisi binadamu, huwa tunafikiri kwa uvivu na urahisi. Huwa tunaona kama vile matokeo yanafuatana. Kwamba baada ya A ni B, kisha C na kuendekea, sivyo mambo yanavyokuwa kwenye uhalisia. Unapaswa kujua kwamba kila jambo hapa duniani lina ugumu na utata. Kuna mambo yatahusishwa ambayo hayakutegemewa (more…)

2752; Niseme vibaya kwenye mengine yote, lakini siyo kwenye hiki kimoja.

By | July 14, 2022

2752; Niseme vibaya kwenye mengine yote, lakini siyo kwenye hiki kimoja. Kama binadamu, najua sijakamilika. Nina maeneo ambayo nina uimara mkubwa. Na maeneo ambayo nina udhaifu mkubwa. Najua kuna watu wananisema vibaya kwenye mambo mbalimbali, mengine ya kweli na mengine siyo ya kweli. Wapo wanaoweza kuwa wanasema sijali, nina roho (more…)