Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (196/366); Tengeneza hali ya mshangao.

By | May 15, 2022

#SheriaYaLeo (196/366); Tengeneza hali ya mshangao. Watoto huwa wana tabia ya kufanya tofauti na kile tunachowaambia wafanye. Lakini kuna hali ambazo watoto huwa wanakuwa tayari kufuata kile wanachoambiwa; pale wanapoahidiwa kitu cha kushangaza. Inaweza kuwa ni zawadi iliyo ndani ya boksi au mchezo ambao mwisho wake hauonekani au safari ambayo (more…)

2691; Umefika mpaka hapo, unaweza kufika mbali zaidi.

By | May 14, 2022

2691; Umefika mpaka hapo, unaweza kufika mbali zaidi. Unapokuwa utajifunza mambo mapya, ni rahisi kuona kama umechelewa sana. Unaweza kujiambia kama ungeyajua hayo mapema basi ungekuwa mbali zaidi. Hali hiyo inaweza kufanya uone huna cha kufanya kwa sasa, kwa sababu umeshapoteza sana. Ni hali inayoweza kukukatisha tamaa. Lakini hivyo sivyo (more…)

#SheriaYaLeo (195/366); Tumia vizuri utofauti.

By | May 14, 2022

#SheriaYaLeo (195/366); Tumia vizuri utofauti. Kuna utofauti ambao wewe unao ukilinganisha na watu wengine. Unapaswa kutumia utofauti huo kuwafanya watu washawishike zaidi na wewe. Na njia bora ya kufanya hivyo ni kuhakikisha mtu unayetaka kumshawishi anajua utofauti huo. Kwanza unamweka kwenye hali ambayo anakosa kile ulichonacho. Kisha unakuja kumpa hicho (more…)

2690; Tatizo siyo kujua.

By | May 13, 2022

2690; Tatizo siyo kujua. Watu wengi huhangaika sana na kutafuta siri za mafanikio. Huwa wanadhani kuna kitu kimefichwa ambacho wakishakijua tu basi mafanikio yatakuwa rahisi kwao. Lakini huo siyo ukweli, Ni njia tu ya watu kujificha na kuukwepa ukweli ambao upo dhahiri. Karibu kila mtu anayetaka kufanikiwa, tayari anajua nini (more…)

#SheriaYaLeo (194/366); Vuruga Matarajio Yao.

By | May 13, 2022

#SheriaYaLeo (194/366); Vuruga Matarajio Yao. Mazoea ni kifo cha ushawishi. Kama watu wanajua kila kitu kuhusu wewe, wameshazoea na kutegemea vitu fulani kutoka kwako, hawawezi kuvutiwa kushawishika na wewe. Wanaona mambo ni yale yale na hakuna cha tofauti. Ili kuendelea kuwa na ushawishi unahitaji kuvuruga matarajio ambayo watu wanayo kwako. (more…)

2689; Hakuna asilimia 100.

By | May 12, 2022

2689; Hakuna asilimia 100. Hakuna kitu chenye ufanisi wa asilimia 100. Hata injini ya gari, pamoja na uwezo mkubwa ambao inakuwa nao, haifikii ufanisi wa asilimia 100. Kuna nguvu nyingi inapotelea kwenye msuguano. Mnyama mkali kama simba ambaye anaweza kuwadhuru karibu wanyama wengine wote wa mwituni, hana ufanisi wa asilimia (more…)

#SheriaYaLeo (193/366); Kutoka urafiki kuwa wapenzi.

By | May 12, 2022

#SheriaYaLeo (193/366); Kutoka urafiki kuwa wapenzi. Kutoka kwenye urafiki mpaka kuwa wapenzi ni kitu kinachoweza kutokea kwa ushawishi usio wa moja kwa moja. Kwanza unaanza kwa mazungumzo ya kirafiki na yule unayemlenga. Mazungumzo hayo yanakupa fursa ya kumjua kiundani, kujua tabia zake, madhaifu yake na yale anayotaka sana. Mbili kwa (more…)

2688; Kipi unachokumbuka?

By | May 11, 2022

2688; Kipi unachokumbuka? Unapokuwa unahangaika na mambo yanayopita, kama habari na mitandao ya kijamii, unaweza kuona kama ni muhimu sana na usipofanya hivyo utapitwa na mengi. Lakini huko ni kujidanganya, Ni kukubali akili yako ikuhadae kwa uvivu ambao akili yako unao. Inajaribu kuepuka mambo magumu na muhimu na kuhangaika na (more…)

#SheriaYaLeo (192/366); Tengeneza habari inayosambaa.

By | May 11, 2022

#SheriaYaLeo (192/366); Tengeneza habari inayosambaa. Pale watu wanapojua kuna kitu unataka, iwe ni kura, kuuza au kukubalika, wanaleta ukinzani. Wanaibuka watu ambao watakupinga kwenye kile ambacho unakitaka. Kuepuka hilo, unapaswa kuficha nia yako nyuma ya tukio ambalo litakuwa habari inayosambaa kwa wengi. Habari hiyo inayosambaa inakamilisha nia yako bila ya (more…)

2687; Ya kwangu ni tofauti.

By | May 10, 2022

2687; Ya kwangu ni tofauti. Kushauri wengine ni rahisi, lakini wewe mwenyewe kutumia ushauri huo huo unaowapa wengine ni ngumu, kwa sababu unaona hali yako ni tofauti. Kuwakosoa na kuwahukumu wengine pale wanapokosea ni rahisi. Lakini pale wewe unapofanya makosa hayo hayo unajitetea kwamba hali yako ni tofauti. Hujihukumu na (more…)