Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (185/366); Usijiangalie mwenyewe, waangalie wengine.

By | May 4, 2022

#SheriaYaLeo (185/366); Usijiangalie mwenyewe, waangalie wengine. Wanaotaka kushawishi wengine huwa hawajiangalii wao wenyewe, bali huwa wanawaangalia zaidi wengine. Hawajiangalii zaidi ndani yao, bali wanaangalia zaidi nje. Hiyo ni kwa sababu kubwa mbili; Moja ni kujiangalia mwenyewe badala ya wengine ni dalili za kutokujiamini. Na pale unapokuwa hujiamini huwezi kuwa na (more…)

2680; Kilicho ndani ya uwezo wako kamili.

By | May 3, 2022

2680; Kilicho ndani ya uwezo wako kamili. Kwenye safari ya mafanikio, huwa kuna kukwamishwa kwa aina mbalimbali. Hasa pale tunapofanya vitu ambavyo vinawategemea wengine, ni rahisi kukwamishwa na hao tunaowategemea. Lakini hupaswi kutumia hilo kama sababu ya kutokufanikiwa. Hupaswi kusema wengine ndiyo waliokukwamisha. Kwani haijalishi ni kipi unategemea mwenyewe, bado (more…)

#SheriaYaLeo (184/366); Usiwaridhishe watu haraka.

By | May 3, 2022

#SheriaYaLeo (184/366); Usiwaridhishe watu haraka. Uwezo wa kuchelewa kuwaridhisha watu una nguvu kubwa kwenye ushawishi. Unawajengea watu hali ya matumaini lakini pia hali ya kukuhitaji zaidi. Ile hali ya kuonekana hutaki sana kitu au hujali sana inakupa wewe nguvu kubwa. Kwani wengine wanasukumwa kukushawishi na kukubembeleza ili uweze kuwapa kile (more…)

Ongea Na Kocha; Getting To Yes, Mtabazi Sahini.

By | May 2, 2022

Habari mwanamafanikio? Karibu kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambapo kuna mambo mawili makubwa. Jambo la kwanza ni mjadala wa kitabu cha GETTING TO YES, kitabu kinachotufundisha msingi sahihi wa kufanya majadiliano yenye manufaa kwa pande zote. Majadiliano hayo ya msingi yana hatua nne ambazo ni kuwatenganisha watu na tatizo, (more…)

2679; Kwamba wewe ni wa pekee sana?

By | May 2, 2022

2679; Kwamba wewe ni wa pekee sana? Tunapojifunza hadhithi za wengine ambao wamepiga hatua, huwa tunafurahia sana hilo. Tunaona wametoka chini na kupambana mpaka kufika juu. Kwa kuangalia nyuma, tunaona wazi kwamba kufanikiwa kwao ilikuwa lazima, hakuna namna wangeweza kushindwa. Lakini sasa inapokuja kwetu, tunaishia kutafuta sababu kwa nini hicho (more…)

#SheriaYaLeo (183/366); Iangalie dunia kwa jicho la ushawishi.

By | May 2, 2022

#SheriaYaLeo (183/366); Iangalie dunia kwa jicho la ushawishi. Ili kuweza kuwa na nguvu ya ushawishi huhitaji kuwa na mabadiliko makubwa kwenye tabia au mwonekano wako. Ushawishi ni mchezo wa kisaikolojia na hivyo kila mtu anaweza kuwa na ubobezi kwenye mchezo huu. Kinachohitajika ni uiangalie dunia kwa utofauti, kupitia jicho la (more…)

2678; Huwezi kuboresha kisichokuwepo.

By | May 1, 2022

2678; Huwezi kuboresha kisichokuwepo. Watu wengi huwa wanakwama kuchukua hatua au kuahirisha kwa sababu wanasubiri ukamilifu. Wanataka wafanye kitu ambacho kimekamilika kabisa na hakina madhaifu yoyote. Lakini hilo ni kinyume na uhalisia. Kompyuta ya kwanza kutengenezwa ilikuwa kubwa ya kujaza chumba kizima, huku uwezo wake wa kubeba kumbukumbu ukiwa mdogo. (more…)

#SheriaYaLeo (182/366); Weka wazi mbinu zako.

By | May 1, 2022

#SheriaYaLeo (182/366); Weka wazi mbinu zako. Pamoja na kwamba ni muhimu kutumia mbinu mbalimbali kuficha nia yako halisi, kuna wakati utalazimika kuweka mbinu na nia yako wazi. Pale watu wanapojua kwamba huwa unatumia mbinu mbalimbali kuficha nia yako, hilo linakosa nguvu. Kwani inakuwa vigumu kwao kuendelea kukuamini. Ni katika hali (more…)

2677; Kutenganishwa na fedha zako.

By | April 30, 2022

2677; Kutenganishwa na fedha zako. Jana mtu wa karibu sana alinipigia simu akinieleza ametapeliwa kiasi fulani cha fedha alichokuwa nacho. Ni wiki moja kabla alinipigia simu akinieleza kiasi cha fedha alichopata na akiwa hana uhakika afanye nini. Ushauri wangu kwake ulikuwa rahisi, nilimwambia hiyo fedha asikimbilie kuitumia kwa namna yoyote (more…)

#SheriaYaLeo (181/366); Iga Maadili Yao.

By | April 30, 2022

#SheriaYaLeo (181/366); Iga Maadili Yao. Kufikiri na kusema kile unachotaka kusema kwa watu wote ni kukitafutia matatizo yasiyo na manufaa. Watu wenye hekima wanajua kwamba wanapaswa kuonyesha tabia zinazoendana na wale wanaowazunguka. Wanajua siyo lazima waamini kwenye mambo hayo. Manufaa wanayopata ni kwa kufanya kile ambacho wengine wanafanya kwa nje, (more…)