Category Archives: KURASA ZA MAISHA

Kila siku mpya kwenye maisha yako ni sawa na ukurasa mpya wa kitabu.
Kwa kila siku mpya unachagua ufanye nini na maisha yako.
Kupitia makala hizi za KURASA ZA MAISHA, utajifunza mambo muhimu ya kufanya ili uwe namaisha bora zaidi.
Makala hizi za kurasa zinakujia kila siku.

2701; Bila msimamo umefika hapo, vipi ukiweka msimamo?

By | May 24, 2022

2701; Bila msimamo umefika hapo, vipi ukiweka msimamo? Pamoja na kukosa msimamo mkubwa kwenye yale unayofanya, umeweza kufika hapo ulipo sasa. Umekuwa hufanyi mambo kwa viwango vya juu kabisa mara zote. Kuna wakati unahamasika na kufanya kwa viwango vya juu. Na kuna wakati mazoea yanakuingia na unafanya kwa mazoea. Pamoja (more…)

2700; Kama wengine wanafanya, usifanye.

By | May 23, 2022

2700; Kama wengine wanafanya, usifanye. Huwezi kupata mafanikio makubwa kama utaendelea kufanya vitu kwa namna ambavyo wengine pia wanavifanya. Ni lazima ufanye vitu tofauti au kwa utofauti na wengine wanavyofanya. Hiyo ni lazima kama unataka kupata mafanikio makubwa. Kamwe usifanye kitu ambacho wengine pia wanakifanya au kwa namna wanavyokifanya. Mara (more…)

2699; Msimamo.

By | May 22, 2022

2699; Msimamo. Kila mtu anajua kile anachopaswa kufanya ili kupata kile anachotaka. Wengi huwanza mpaka kuchukua hatua hizo. Lakini bado wengi hawafanikiwi. Kwa sababu wanachokosa ni msimamo. Hawafanyi jambo kwa kujirudia rudia kwa muda mrefu. Wanapoona matokeo hayaji haraka kama wanavyotaka, wanaacha kufanya. Msimamo kwenye ufanyaji ni moja ya mahitaji (more…)

2698; Majuto hayana nafasi.

By | May 21, 2022

2698; Majuto hayana nafasi. Kuna fursa ulishindwa kuitumia kipindi cha nyuma na hivyo kushindwa kunufaika nayo. Badala ya kupoteza muda wako kwenye kujutia hilo, unapaswa kulitumia kama funzo la kutokubali kukosa fursa nyingine nzuri. Kuna makosa uliyafanya huko nyuma ambayo yalikugharimu sana. Badala ya kupoteza muda kwenye kujutia makosa hayo, (more…)

2696; Ukilinganisha na nini?

By | May 19, 2022

2696; Ukilinganisha na nini? Utawasikia watu wakisema, maisha ni magumu. Na hapo unaweza kujiuliza ukilinganisha na nini? Je maisha ni magumu ukilinganisha na kifo? Au maisha ni magumu ukilinganisha na maumivu makali mtu unayopata ukiwa unaumwa? Kama upo hai na huna maradhi yanayokuumiza kila wakati, maisha siyo magumu kama unavyojiambia. (more…)

2695; Malengo madogo ndiyo yanayokuchelewesha.

By | May 18, 2022

2695; Malengo madogo ndiyo yanayokuchelewesha. Rafiki, watu huwa wanadhani kwamba ukiweka malengo makubwa halafu usiyafikie basi umeshindwa. Hiyo siyo kweli, ukiweka malengo makubwa kabisa na usiyafikie, bado wewe ni mshindi. Kwa sababu utakachokuwa umepata siyo sawa na ambacho ungepata kama usingekuwa umeweka malengo hayo makubwa. Kushindwa ni pale unapoweka malengo (more…)

2694; Ukiwa njia panda, chagua njia ngumu.

By | May 17, 2022

2694; Ukiwa njia panda, chagua njia ngumu. Mara kwa mara huwa tunajikuta njia panda, tukiwa na machaguo mengi na hatujui tuchague lipi. Hapa ndipo wengi huwa wanakwama kwa kushindwa kujua kipi sahihi kwao kuchagua. Wanatumia muda mrefu kuchambua mambo bila kuchagua. Na hata pale wanapofikia hatua ya kuchagua basi hukimbilia (more…)

2693; Haiwezekani kwa sababu hujafanya.

By | May 16, 2022

2693; Haiwezekani kwa sababu hujafanya. Wakati Wright Brothers wanahangaika kufanya majaribio ya kurusha ndege, wanasayansi wakubwa walisema wazi kwamba binadamu hawataweza kutusha ndege kwa miaka 100 ijayo. Kanuni zote za kisayansi zilionyesha hicho ni kitu kisichowezekana. Lakini mwaka mmoja baadaye Wright Brothers walirusha ndege yao na mengine yakabaki historia. Kabla (more…)