Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (225/366); Tumia hisia zao.

By | June 13, 2022

#SheriaYaLeo (225/366); Tumia hisia zao. Kama unataka kumshawishi mtu abadilike, usipingane na hisia zake, bali zitumie hizo kuchochea mabadiliko. Kama mtu ni mkorofi na mtukutu, badala ya kuyapinga hayo, mweke kwenye hali ya kutaka kubadilika ili kuonyesha ukorofi na utukutu wake. Kwa kuyafanya mabadiliko yaendane na kile ambacho tayari mtu (more…)

#SheriaYaLeo (224/366); Bobea sanaa ya maigizo.

By | June 12, 2022

#SheriaYaLeo (224/366); Bobea sanaa ya maigizo. Huwezi kufanikiwa kwenye kuwashawishi wengine bila kubobea kwenye lugha na sanaa ya maigizo. Lazima uweze kupenyeza maneno yenye ushawishi wakati wa mazungumzo na wengine. Yanakuwa ni maneno ambayo wengine hawayatarajii, lakini yanajenga ushawishi mkubwa kwao. Ili maneno hayo yawe na nguvu ya ushawishi unapaswa (more…)

#SheriaYaLeo (223/366); Nasa Ufahari wao.

By | June 11, 2022

#SheriaYaLeo (223/366); Nasa Ufahari wao. Kila mtu huwa ana ufahari au majigambo ndani yake. Hali ya kujiona ni muhimu kwenye hii dunia. Pale mtu anapokushambulia na hujui ni kwa nini, mara nyinyi ni kwa sababu unakuwa umetishia ufahari wao. Mara zote unapaswa kuhakikisha watu wanajisikia vizuri kuhusu wao wenyewe kwa (more…)

#SheriaYaLeo (222/366); Waonjeshe dawa yao wenyewe.

By | June 10, 2022

#SheriaYaLeo (222/366); Waonjeshe dawa yao wenyewe. Kama ambavyo tumeshaona, mabishano huwa hayafanyi kazi. Kuwaambia watu kile wanachokosea hakuwafanyi wajirekebishe. Badala yake watajitetea na kuendelea kukifanya. Njia bora ya kuwapa funzo ili wabadilike ni kuwaonjesha dawa yao wenyewe. Hapo unachofanya ni kuwafanyia kile ambacho wamekufanyia wewe, kwa namna ambavyo wamekifanya. Unakifanya (more…)

#SheriaYaLeo (221/366); Epuka Mabishano.

By | June 9, 2022

#SheriaYaLeo (221/366); Epuka Mabishano. Mabishano huwa hayana manufaa yoyote. Hiyo ni kwa sababu kila mtu huwa anaamini maoni yake ni sahihi zaidi. Hivyo unavyobisha na kupinga maoni ya mtu, humshawishi, bali unamfanya azidi kuamini maoni yake. Kadiri unavyombishia mtu ndivyo anavyoacha kukusikiliza na kusimamia upande wake. Kama unataka kuwashawishi watu (more…)

#SheriaYaLeo (220/366); Zingatia maslahi yao binafsi.

By | June 8, 2022

#SheriaYaLeo (220/366); Zingatia maslahi yao binafsi. Njia ya haraka na ya uhakika ya kuteka akili za watu na kuwashawishi ni kuwaonyesha jinsi ambavyo kitu kinakwenda kuwanufaisha wao wenyewe. Maslahi binafsi ndiyo nguvu yenye msukumo mkubwa kwa wengi. Tukio muhimu linaweza kuwahamasisha watu mwanzoni. Lakini baada ya hamasa hiyo ya mwanzo (more…)

#SheriaYaLeo (219/366); Waweke kwenye hali ya kudhani.

By | June 7, 2022

#SheriaYaLeo (219/366); Waweke kwenye hali ya kudhani. Ili kuwafanya wengine wakufuatilie na hivyo kuweza kuwashawishi, unapaswa kuwaweka kwenye hali ya kudhani. Usiwape uhakika kwa kujua kila kitu kuhusu wewe.Kwani watu wakishakijua kitu na kuwa na uhakika nacho huwa wanakizoea, wanakichoka na kuacha kukifuatilia. Watu huwa wanachoshwa haraka sana na kitu (more…)

#SheriaYaLeo (218/366); Shinda kwa kutumia vitendo na siyo maneno.

By | June 6, 2022

#SheriaYaLeo (218/366); Shinda kwa kutumia vitendo na siyo maneno. Watu wengi huwa wanakazana sana kutumia maneno kwenye kuwashawishi wengine. Lakini watu huwa ni wagumu sana kushawishika na kubadilika kwa kutumia maneno. Kwa watu, matendo yana nguvu na ushawishi mkubwa kuliko maneno. Hivyo pale inapowezekana kutumia vitendo, usihangaike sana na maneno. (more…)

#SheriaYaLeo (217/366); Tumia hisia kali.

By | June 5, 2022

#SheriaYaLeo (217/366); Tumia hisia kali. Pale unapotaka kuonyesha msisitizo wa kitu na kuwa na ushawishi mkubwa, unapaswa kutumia hisia kali. Hisia kali, hasa za chuki huwa zinaeleweka sana na kuwashawishi wengine. Hiyo ni kwa sababu zinakuwa ni hisia walizonazo ila hawathubutu kuziweka wazi. Hivyo pale wewe unapoziweka wazi, wanakuona kama (more…)

#SheriaYaLeo (216/366); Wazungumzie wao na kuwasifia.

By | June 4, 2022

#SheriaYaLeo (216/366); Wazungumzie wao na kuwasifia. Huwa tunajaribu kuwashawishi watu kwa kueleza sifa zetu na makubwa ambayo tumeyafanya. Tunaahidi makubwa zaidi ambayo tunakwenda kuyafanya. Na pia tunaomba wengine watusaidie kwa namna mbalimbali. Tunachosahau ni kwamba kufanya yote hayo tunakuwa tumeweka umakini wote kwetu wenyewe. Kwenye dunia ambayo kila mtu anajifikiria (more…)