Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (163/366); Mwondoe mwenye ushawishi.

By | April 12, 2022

#SheriaYaLeo (163/366); Mwondoe mwenye ushawishi. Kwenye kundi lolote lile huwa kuna mtu mmoja mwenye ushawishi mkubwa na ambaye wengine wote wanamsikiliza. Na hata kunapokuwa na matatizo, chanzo chake kikuu huwa ni mtu mmoja mwenye ushawishi. Pale anapokuwa hajaridhika kwa namna fulani anakuwa tayari kusambaza hilo kwa wengine na kuwa chanzo (more…)

#SheriaYaLeo (162/366); Waambukize watu hisia chanya.

By | April 11, 2022

#SheriaYaLeo (162/366); Waambukize watu hisia chanya. Sisi binadamu ni viumbe wa kihisia. Unapokuwa ndani ya kundi lolote lile, hasa kama kiongozi, waambukize watu hisia chanya kwa kuwapa hamasa ya kuweza kufanya makubwa zaidi. Washirikishe maono makubwa na malengo ya kufika kwenye maono hayo. Waonyeshe ung’ang’anizi katika kufikia maono hayo. Pia (more…)

#SheriaYaLeo (161/366); Wafanye watu wajisikie wako juu.

By | April 10, 2022

#SheriaYaLeo (161/366); Wafanye watu wajisikie wako juu. Watu wanapenda sifa na kutukuzwa, wanapenda kuona wapo juu na wengine wanawategemea kwa mambo mbalimbali. Pale unapotaka kitu kutoka kwa watu, hasa wale wenye mamlaka, wafanye wajione wako juu. Wafanye waone upo chini yao na unawategemea sana kwa kile unachotaka. Hilo linawafanya wajione (more…)

#SheriaYaLeo (160/366); Wavuruge wasijue nia yako halisi.

By | April 9, 2022

#SheriaYaLeo (160/366); Wavuruge wasijue nia yako halisi. Kwa chochote unachotaka, kuna watu ambao ni kikwazo kwako, ambao wapo tayari kukuzuia usikipate. Njia bora ya kuwavuka watu hao na kupata kile unachotaka ni kuwavuruga. Unawavuruga kwa kuwahadaa, kuwafanya waone unataka kitu kingine ambacho siyo nia yako halisi. Kwa njia hii huendei (more…)

#SheriaYaLeo (159/366); Usidharau akili za wengine.

By | April 8, 2022

#SheriaYaLeo (159/366); Usidharau akili za wengine. Huwa hatupendi kukubali kwamba wengine wana akili kuliko sisi. Tunapokutana na watu wenye akili sana, huwa tunatafuta kila njia ya kujitetea ili kuonyesha kwamba hatupo nyuma. Tutasema wana akili za darasani tu. Au wana akili kwa sababu walisoma shule za gharama kubwa. Au wana (more…)

#SheriaYaLeo (158/366); Igiza nafasi yako vizuri.

By | April 7, 2022

#SheriaYaLeo (158/366); Igiza nafasi yako vizuri. Maisha ni maigizo, kile ambacho watu wanaonyesha kwa nje, sivyo walivyo ndani yao. Hivyo moja ya wajibu wako mkubwa kwenye maisha ni kuigiza nafasi yako vizuri. Hasa kwenye eneo la hisia, lazima uweze kuvaa hisia sahihi kwa wakati sahihi. Pale unapohitajika kuwa na hisia (more…)

#SheriaYaLeo (157/366); Waweke watu kwenye shauku ya kukufuatilia.

By | April 6, 2022

#SheriaYaLeo (157/366); Waweke watu kwenye shauku ya kukufuatilia. Watu huwa wanapenda kufuatilia vitu ambavyo vinawaweka juu juu. Vitu ambavyo hawana uhakika vitakwendaje. Vitu ambavyo ni tofauti kabisa na mazoea na hivyo havitabiriki. Kwa kila unachofanya, kifanye kwa namna hiyo na siyo kwa mazoea. Wafanye watu wawe wanajiuliza kipi kingine utafanya (more…)

#SheriaYaLeo (156/366); Tumia udhaifu wa watu kuamini mwonekano wa nje.

By | April 5, 2022

#SheriaYaLeo (156/366); Tumia udhaifu wa watu kuamini mwonekano wa nje. Ni asili yetu binadamu kuamini kwa haraka kile ambacho tunakiona. Huwa hatuna muda wa kuchunguza kwa undani na kujua nia halisi ya mtu. Hivyo unaweza kutumia udhaifu huu kukubalika na wengine na kupata kile unachotaka. Unachopaswa kufanya ni kutengeneza mwonekano (more…)

#SheriaYaLeo (155/366); Dhibiti mwonekano wako.

By | April 4, 2022

#SheriaYaLeo (155/366); Dhibiti mwonekano wako. Kwenye maisha watu wanakuhukumu na kukuchukulia kutokana na mwonekano wako. Kwa kuwa watu hawana muda wa kuchunguza kwa ndani, wanachukulia mwonekano wako wa nje ndivyo ulivyo kwa ndani. Ili watu wakuchukulie kwa namna sahihi kwako, unapaswa kutengeneza mwonekano wa nje ambao unawajengea picha hiyo. Jiweke (more…)

#SheriaYaLeo (154/366); Tumia uhaba kuongeza thamani.

By | April 3, 2022

#SheriaYaLeo (154/366); Tumia uhaba kuongeza thamani. Ni kanuni ya msingi kabisa ya uchumi kwamba kitu kinapopatikana kwa wingi, thamani yake inapungua na hivyo bei yake kuwa chini. Lakini kitu kinapopatikana kwa uhaba, thamani yake inakuwa kubwa na bei yake kuwa juu. Ili kuongeza thamani yako binafsi na ya kile unachofanya, (more…)