Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (173/366); Chukua mamlaka tararibu.

By | April 22, 2022

#SheriaYaLeo (173/366); Chukua mamlaka tararibu. Ukionekana una haraka sana ya kuchukua mamlaka, utaishia kuibua hasira, wivu na chuki. Watu hawatakuwa tayari kukuachia uchukue mamlaka kwa vile unavyotaka. Hivyo njia bora ni kuchukua mamlaka hayo taratibu. Kujipa muda wa kutosha katika kukamilisha hilo. Kwanza wape watu nafasi ya kuona wanafanya kwa (more…)

#SheriaYaLeo (172/366); Onyesha udhaifu wako.

By | April 21, 2022

#SheriaYaLeo (172/366); Onyesha udhaifu wako. Jifunze kugeuza udhaifu wako kuwa njia ya kupata mamlaka. Pale unapoonekana imara na mkamilifu wakati wote, watu wanaweza kuona wewe siyo wa aina yao. Katika nyakati fulani unapaswa kuwaonyesha watu udhaifu wako ili waweze kuona wewe ni kama wao, na kukuamini zaidi. Hila linakufanya uwe (more…)

#SheriaYaLeo (171/366); Wafanye wengine waje kwako.

By | April 20, 2022

#SheriaYaLeo (171/366); Wafanye wengine waje kwako. Pale unapoonekana kuwahitaji sana wengine na kwenda kuwafuata, unaishia kuonekana wa kawaida na hakuna anayekuthamini. Lakini pale unapowafanya watu waje kwako, kwa kuwa siyo rahisi wewe kupatikana, unakuwa wa tofauti na unathaminika. Kwa chochote unachofanya, wafanye watu waje kwako wakiwa na uhitaji. Wafanye waje (more…)

#SheriaYaLeo (170/366); Usifanye mabadiliko makubwa kwa wakati mmoja.

By | April 19, 2022

#SheriaYaLeo (170/366); Usifanye mabadiliko makubwa kwa wakati mmoja. Sisi binadamu huwa tunapenda kusikia kuhusu mabadiliko, ila huwa hatupo tayari kubadilika. Watu wanajua kabisa umuhimu wa mabadiliko kwenye taasisi na hata mtu mmoja mmoja. Lakini pale mabadiliko hayo yanapowahusu wao binafsi na kuathiri maslahi yao huwa hawayafurahii. Mabadiliko ni mazuri na (more…)

#SheriaYaLeo (169/366); Tumia mwonekano kushawishi.

By | April 18, 2022

#SheriaYaLeo (169/366); Tumia mwonekano kushawishi. Watu huwa wanashawishika sana na mwonekano wa vitu ulivyo. Vitu kama rangi, muundo na mpangilio wa vitu vina nguvu ya kuwashawishi watu kwa namna fulani. Kwa mfano matumizi ya rangi nyekundu kwenye maandishi yanawafanya watu waone kitu ni muhimu na cha haraka hivyo kushawishika kuchukua (more…)

#SheriaYaLeo; (168/366); Dhibiti machaguo unayowapa watu.

By | April 17, 2022

#SheriaYaLeo; (168/366); Dhibiti machaguo unayowapa watu. Watu huwa wanapenda kuona wana uhuru wa kuchagua mambo yao wenyewe. Lakini machaguo yanapokuwa mengi, huwa inakuwa vigumu kwa mtu kuweza kuchagua. Anajikuta njia panda na kushindwa kuchagua kitu kimoja. Ili kuwasaidia watu kufanya maamuzi na wewe kuweza kupata kile unachotaka, dhibiti machaguo unayowapa (more…)

#SheriaYaLeo (167/366); Tumia sanaa ya kuwepo na kutokuwepo.

By | April 16, 2022

#SheriaYaLeo (167/366); Tumia sanaa ya kuwepo na kutokuwepo. Unapaswa kujua jinsi ya kupangilia kuwepo na kutokuwepo kwako. Sisi binadamu huwa tunadharau kitu kinachopatikana muda wote na kuthamini kile ambacho hakipatikani. Kwa ujumla, ni vyema kuegemea zaidi upande wa kutokuwepo/kutokupatikana ili pale unapokuja kuonekana watu wanakuwa na shauku kubwa. Ukifanya hilo, (more…)

#SheriaYaLeo (166/366); Kuwa mkali.

By | April 15, 2022

#SheriaYaLeo (166/366); Kuwa mkali. Mara nyingi huwa tunapenda kuwa wapole na wenye kujali wengine ili kuweza kuendana nao vizuri na kupata kile tunachotaka. Hili huwa linafanya kazi vizuri wakati wa kawaida. Lakini wakati wa hatari hilo linakuwa mzigo kwako, kufanya hivyo kunapelekea watu wakuone ni mtu unayefaa kuonewa, kukatishwa tamaa (more…)

#SheriaYaLeo (165/366); Ongoza ukiwa mbele.

By | April 14, 2022

#SheriaYaLeo (165/366); Ongoza ukiwa mbele. Unapokuwa kiongozi, unahitaji kuwa na ushawishi mkubwa kwa wale unaowaongoza ili wafanye yale wanayopaswa kufanyika. Huwezi kupata ushawishi huo kwa kulazimisha au kubembeleza. Hizo ni njia zenye matokeo ya muda mfupi ila siyo endelevu. Njia bora ya kuwa na ushawishi kwa wale unaowaongoza ni kuwa (more…)

#SheriaYaLeo (164/366); Tumia mbinu ya kujisalimisha.

By | April 13, 2022

#SheriaYaLeo (164/366); Tumia mbinu ya kujisalimisha. Unapokuwa dhaifu, usipambane na mwenye nguvu. Badala yake chagua kujisalimisha. Kupambana na mwenye nguvu huku wewe ukiwa dhaifu ni kuchagua kushindwa vibaya. Kujisalimisha kunakupa nafasi ya kujipanga na kukusanya nguvu zako ili baadaye uweze kushambulia na kushinda. Kujisalimisha kunamfanya adui yako akudharau na kukuona (more…)