#SheriaYaLeo (305/366); Wewe ndiyo kikwazo kwako.

By | September 1, 2022

#SheriaYaLeo (305/366); Wewe ndiyo kikwazo kwako. Maisha ni vita na mapambano, kila wakati unajikuta ukikabiliana na hali mbaya, mahusiano mabovu na mashirikiano hatari. Jinsi unavyokabiliana na hali hizo ndiyo itaamua hatima yako. Kama utajiona umepotea, kama utapoteza mwelekeo, kama huwezi kutofautisha rafiki na adui, unapaswa kujilaumu mwenyewe. Kila kitu kwenye (more…)

2800; Ushahidi mwingine kwamba biashara siyo mtaji pekee.

By | August 31, 2022

2800; Ushahidi mwingine kwamba biashara siyo mtaji pekee. Biashara kuu ya benki ni kutoa mikopo kwa watu, ambao watailipa kwa riba. Hivyo ndivyo benki zinaingiza faida. Sehemu kubwa ya mikopo ambayo benki nyingi zinatoa ni ya biashara au uwekezaji. Mtu anachukua mkopo kwenda kukuza zaidi biashara yake, kuongeza faida na (more…)

#SheriaYaLeo (304/366); Asili ya binadamu haibadiliki.

By | August 31, 2022

#SheriaYaLeo (304/366); Asili ya binadamu haibadiliki. Dunia inaendelea kupiga hatua. Maendeleo ya sayansi na teknolojia yanaleta ufahamu kwenye mambo mengi ambayo huko nyuma hayakujulikana. Kwa sababu hiyo tunaweza kudhani pia kwamba binadamu nao wanabadilika. Lakini ukweli ni kwamba asili ya binadamu huwa haibadiliki. Bado watu wanafanya maamuzi kwa hisia badala (more…)

#SheriaYaLeo (303/366); Dhibiti majivuno yako.

By | August 30, 2022

#SheriaYaLeo (303/366); Dhibiti majivuno yako. Unataka kufanya makubwa na kupata mafanikio makubwa kwenye maisha yako. Umejiwekea malengo makubwa ambayo una uhakika wa kuyafikia. Hayo yote ni mazuri kabisa na ndivyo wengi waliofanikiwa walivyofanya. Ila kuna mahali pamoja wengi hukosea na hilo kupelekea kushindwa. Wanapoweka malengo yao makubwa, wanaona ni lazima (more…)

2798; Mazoezi na vita.

By | August 29, 2022

2798; Mazoezi na vita. Kabla ya wanajeshi kwenda vitani huwa wanafanya mazoezi makali. Mazoezi ambayo yanajaribu kuiga uhalisia wa yale watakayokutana nayo kwenye vita. Kabla wachezaji hawajaingia kwenye mashindano, huwa wanafanya mazoezi makali. Mazoezi hayo hugusa kila hali ambayo watakutana nayo kwenye mashindano. Mazoezi yana nguvu ya kumjengea mtu uzoefu (more…)

#SheriaYaLeo (302/366); Sogelea unachokionea wivu.

By | August 29, 2022

#SheriaYaLeo (302/366);Sogelea unachokionea wivu. Watu huwa wana tabia ya kuficha matatizo yao na kuonyesha nyuso zenye furaha. Tunachoona na kusikia kwa watu ni habari njema na ushindi. Hilo huwa linajenga hali ya wivu kwetu, kwa kuona wengine wapo pazuri kuliko pale tulipo sisi. Lakini kama tutawasogelea karibu hao tunaowaonea wivu, (more…)

#SheriaYaLeo (301/366); Ona kivuli chako.

By | August 28, 2022

#SheriaYaLeo (301/366); Ona kivuli chako. Kila mtu huwa ana pande mbili. Upande mzuri ambao ndiyo anauonyesha kwa wengine. Na upande mbaya ambao anauficha. Wengi wakiwa hadharani hufanya mambo mazuri na ya kupendeza. Lakini wakiwa faraghani hufanya mambo mabaya na yasiyo ya kupendeza. Na mara nyingi, wale wanaojionyesha ni wema sana (more…)

2796; Uhakika kwamba unaweza kufanikiwa.

By | August 27, 2022

2796; Uhakika kwamba unaweza kufanikiwa. Thomas Edison amewahi kunukuliwa akisema; “Kama tungefanya mambo yote tunayoweza kufanya, tungejishangaza wenyewe.” Sina cha kuongeza hapo, tunaenda moja kwa moja kwenye hatua ya kuchukua. Hatua ya kuchukua; Chukua kalamu na karatasi na orodhesha mambo yote unayoweza kufanya kwenye biashara au kazi yako. Orodhesha yote (more…)