#SheriaYaLeo (300/366); Kataa maelezo rahisi.

By | August 27, 2022

#SheriaYaLeo (300/366); Kataa maelezo rahisi. Sisi binadamu huwa tuna ukomo fulani kwenye uwezo wetu wa kufikiri ambao ndiyo chanzo cha matatizo mengi tunayokutana nayo. Tunapofikiria kuhusu watu au kitu ambacho kimetokea, huwa tunakimbilia kwenye maelezo rahisi kwetu kuelewa. Huwa tunakimbilia kwenye kuangalia kama mtu au kitu ni kizuri au kibaya, (more…)

#SheriaYaLeo (299/366); Chunguza mizizi ya hisia zako.

By | August 26, 2022

#SheriaYaLeo (299/366); Chunguza mizizi ya hisia zako. Kila hisia unazokuwa nazo, huwa zinakuwa na mizizi yake ambayo huwa haionekani wazi. Ni mpaka uchunguze kwa kina ndiyo utaweza kujua chanzo halisi cha hisia unazokuwa nazo. Kwa mfano umepatwa na hasira, unapaswa kuacha hisia hizo zitulie, kisha kuchunguza nini kimezisababisha. Kama zimesababishwa (more…)

#SheriaYaLeo (298/366); Jua hujui.

By | August 25, 2022

#SheriaYaLeo (298/366); Jua hujui. Huwa tunapenda kuwabeza watu wa zama zilizopita jinsi ambavyo hawakuwa wanajua yale ambayo tunajua sasa. Tunaona kama walikuwa watu wajinga na walioshindwa kujua yale ya msingi. Hebu fikiria ni kwa namna gani watu wa vizazi vijavyo watatushangaa na kutubeza kwa mambo tunayofanya sasa. Kuna mengi tunajua, (more…)

2793; Eneo lako la nguvu.

By | August 24, 2022

2793; Eneo lako la nguvu. Jamii huwa inapenda kuwadhibiti na kuwatawala watu. Na ili kuhakikisha hilo linafanikiwa, hatua kubwa na ya kwanza ambayo jamii huwa inafanya ni kuhakikisha mtu hawi yeye. Kwa sababu inajua mtu ana nguvu na mamlaka makubwa sana pale anapokuwa yeye, anapokuwa halisi kwake. Hivyo inakuondoa kwanza (more…)

#SheriaYaLeo (297/366); Nafsi iliyopotea.

By | August 24, 2022

#SheriaYaLeo (297/366); Nafsi iliyopotea. Kila mtu huwa ana nafsi yake ambayo ameipoteza. Hilo linatokana na mtu kuchagua kuwa kama vile ambavyo watu wanataka awe na siyo kama anavyosukumwa kuwa kutoka ndani yake. Wajibu wako mkubwa kwenye maisha ni kuondokana na hali ya mgando unayokuwa nayo, vile unavyojiweka ili kuwaridhisha wengine. (more…)

2792; Umewafundisha?

By | August 23, 2022

2792; Umewafundisha? Kama watu hawafanyi kitu, kuna sababu mbili tu; HAWAWEZI au HAWATAKI. Wanakuwa hawawezi pale wanapokuwa hawajui jinsi ya kufanya kitu hicho. Hilo linakuwa gumu kwao kufanya. Na mbaya zaidi, watu huwa hawapendi kukiri kwamba hawajui. Hivyo hujifanya wanajua, lakini kutokujua kwao kunakuwa kikwazo kwenye ufanyaji. Hapo hujaweka hali (more…)

#SheriaYaLeo (296/366); Usipotezwe na vitu visivyo na tija.

By | August 23, 2022

#SheriaYaLeo (296/366); Usipotezwe na vitu visivyo na tija. Kuna wakati unajikuta umezidiwa na majukumu ambayo unapaswa kuyatekeleza. Unajikuta ukiwa na mambo mengi ya kufanya, lakini muda wa kuyafanya unakuwa mdogo. Ni katika wakati huo ndiyo unapata hali ya kuvurugwa, kwa kuona kuna mambo unapoteza au unayakosa kwa sababu umepoteza udhibiti. (more…)

2791; Uwanja wa nyumbani.

By | August 22, 2022

2791; Uwanja wa nyumbani. Kwenye michezo yote, huwa kuna dhana ya uwanja wa nyumbani. Kwamba timu inakuwa kwenye nafasi nzuri ya kushinda inapokuwa inacheza kwenye uwanja wa nyumbani. Hivyo timu inapokuwa inacheza uwanja wa ugenini, huko hucheza kwa kujilinda zaidi ili isifungwe. Timu ikiwa ugenini haiangalii sana kusinda, bali inakazana (more…)