2675; Haifanyi kazi…

By | April 28, 2022

2675; Haifanyi kazi… Umejifunza njia za masoko za kuongeza wateja kwenye biashara yako. Unatumia njia hizo, lakini bado wateja hawaongezeki. Umejifunza njia ya kupunguza uzito wa mwili ni kula kwa afya na kufanya mazoezi. Umefanya hivyo, lakini bado uzito haupungui. Umejifunza njia ya kufika kwenye utajiri mkubwa ni kuweka akiba (more…)

#SheriaYaLeo (179/366); Waambie watu wanachotaka kusikia.

By | April 28, 2022

#SheriaYaLeo (179/366); Waambie watu wanachotaka kusikia. Ukweli huwa unauma, Watu wengi huwa hawapendi kusikia ukweli. Hivyo kama unataka kupata wafuasi wengi, usiwaambie watu ukweli, bali waambie kile wanachotaka kusikia. Watu hawataki kusikia kwamba kujenga utajiri kunahitaji muda, juhudi na nidhamu ya hali ya juu. Wanataka kusikia wakipanda pesa leo kesho (more…)

2674; Uongozi ni kuwaudhi watu kwa manufaa yao wenyewe.

By | April 27, 2022

2674; Uongozi ni kuwaudhi watu kwa manufaa yao wenyewe. Kama hutaki kuwaudhi watu. Basi usiwe kiongozi. Kwa sababu wajibu mkubwa wa kiongozi ni kuwafanya watu wafanye vitu ambavyo hawataki kufanya, ila vina manufaa kwao. Yaani kitu kina manufaa kwa mtu, lakini hataki kukifanya, kwa sababu ni kipya kwake au kigumu. (more…)

#SheriaYaLeo (178/366); Kamwe usifanye kwa mazoea.

By | April 27, 2022

#SheriaYaLeo (178/366); Kamwe usifanye kwa mazoea. Unapokuwa kijana huwa ni rahisi kuchukua hatua za tofauti. Japo zinaweza kuwa hatari, lakini ndiyo zinazoleta matokeo makubwa na ya tofauti. Lakini kadiri umri unavyokwenda, unaanza kufanya zaidi kwa mazoea badala ya kujaribu vitu vipya. Kutokana na umri kwenda, unaepuka hatua ambazo ni hatari (more…)

2673; Huo muda unaupata wapi?

By | April 26, 2022

2673; Huo muda unaupata wapi? Kama kuna changamoto unazopitia kwenye maisha yako, lakini bado pia unahangaika na mambo yasiyokuwa na tija, ni jambo la kushangaza. Kama una ndoto kubwa ambazo bado hujazifikia, lakini una mambo yasiyohusiana na ndoto hizo ambayo yanakutinga, ni vigumu kueleweka. Unapokuwa na changamoto zinazokukabili, inapaswa muda (more…)

#SheriaYaLeo (177/366); Tengeneza hali ya usiri.

By | April 26, 2022

#SheriaYaLeo (177/366); Tengeneza hali ya usiri. Watu wanapoelewa na kuzoea mtu au kitu huwa wanakidharau. Hiyo ni kwa sababu hakuna chochote kinachokuwa kinawasukuma kufuatilia ili kujua zaidi. Kama unataka watu wakufuatilie, tengeneza hali ya usiri. Fanya mambo ambayo watu hawayaelewi au hawawezi kuyaelezea. Kuwa na mwonekano wa tofauti ambao watu (more…)

Ongea Na Kocha; How To Live On 24 Hours A Day Na Mwongozo Wa Kufanya Tathmini Ya Robo Mwaka.

By | April 25, 2022

Habari Mwanamafanikio? Karibu kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambacho kina mambo mawili makubwa. Jambo la kwanza ni mjadala wa kitabu cha HOW TO LIVE ON 24 HOURS A DAY kilichoandikwa na Arnold Bennett. Kitabu hiki kifupi ambacho kimeandikwa zaidi ya miaka 100 iliyopita kina mengi ya kutufundisha kuhusu matumizi (more…)

2672; Una matokeo yapi ya kuonyesha?

By | April 25, 2022

2672; Una matokeo yapi ya kuonyesha? Kila mmoja wetu ana mambo mengi sana ambayo amewahi kuyafanya kwenye maisha yake. Fursa mbalimbali ambazo amekimbizana nazo akiamini hizo ndiyo zitampa kila kitu. Lakini kabla hata fursa moja haijalipa, au pale anapokutana na changamoto, haraka sana anakimbilia kwenye fursa nyingine. Hiyo ndiyo imekuwa (more…)

#SheriaYaLeo (176/366); Tumia maneno matupu.

By | April 25, 2022

#SheriaYaLeo (176/366); Tumia maneno matupu. Watu huwa wanapenda na hata kuelewa zaidi lugha ya picha. Hiyo ni kwa sababu inawawezesha kujenga taswira ya kitu na kukielewa vizuri. Unapotaka kuwahadaa watu, nenda kinyume na hilo. Tumia lugha ya maneno matupu ambayo hayamwezeshi mtu kujenga taswira yoyote. Lugha ya aina hiyo inamfanya (more…)

2671; Wana ndoto, wasaidie wazifikie.

By | April 24, 2022

2671; Wana ndoto, wasaidie wazifikie. Falsafa kuu ya KISIMA CHA MAARIFA ni unawesa kupata chochote unachotaka kama utawasaidia wengi zaidi kupata kile wanachotaka. Ndiyo, kuna vitu tunavitaka, ila kuvipata ni mpaka kwanza tuwasaidie wengine kupata vile wanavyotaka. Kila mtu hapa duniani ana ndoto mbalimbali anazotaka kuzifikia. Kwenye kila eneo la (more…)