#SheriaYaLeo (175/366); Jinsi ya kuwafanya watu wawe tayari kukusaidia.

By | April 24, 2022

#SheriaYaLeo (175/366); Jinsi ya kuwafanya watu wawe tayari kukusaidia. Kama unataka watu wakusaidie kitu fulani, usiwakumbushe jinsi ambavyo wewe umewahi kuwasaidia huko nyuma. Unaweza kudhani kwa kuwakumbusha hilo wataona wanapaswa kulipa fadhila na hivyo kusukumwa kukusaidia. Lakini siyo kinachotokea. Unapowakumbusha watu jinsi ulivyowasaidia huko nyuma unawafanya wajione hawajiwezi na wanategemea (more…)

#SheriaYaLeo (174/366); Dhibiti kile unachosema.

By | April 23, 2022

#SheriaYaLeo (174/366); Dhibiti kile unachosema. Mamlaka ni mchezo wa mwonekano kadiri unavyozungumza kidogo, ndivyo unavyoonekana wa muhimu na mwenye mamlaka makubwa. Unapokaa kimya unawafanya wengine washindwe kukutabiri. Maana sisi binadamu ni mashine za kutengeneza maana, huwa hatuwezi kutulia kama hatujui maana au nia ya kitu fulani. Unapozungumza sana, unaweka kila (more…)

2669; Nini ni sahihi na siyo nani yuko sahihi.

By | April 22, 2022

2669; Nini ni sahihi na siyo nani yuko sahihi. Changamoto kubwa tunazokutana nazo kwenye maisha huwa zinaanzia kwenye hukumu tunazotoa kwa wengine. Mara nyingi hukumu hizo huwa ni za upendeleo. Kama mtu tunampenda au kukubaliana naye tunamhukumu vizuri kwa sababu tunaona upande wake mzuri tu. Na kama mtu hatumpendi au (more…)

#SheriaYaLeo (173/366); Chukua mamlaka tararibu.

By | April 22, 2022

#SheriaYaLeo (173/366); Chukua mamlaka tararibu. Ukionekana una haraka sana ya kuchukua mamlaka, utaishia kuibua hasira, wivu na chuki. Watu hawatakuwa tayari kukuachia uchukue mamlaka kwa vile unavyotaka. Hivyo njia bora ni kuchukua mamlaka hayo taratibu. Kujipa muda wa kutosha katika kukamilisha hilo. Kwanza wape watu nafasi ya kuona wanafanya kwa (more…)

2668; Haya mambo huwezi kuyalazimisha.

By | April 21, 2022

2668; Haya mambo huwezi kuyalazimisha. Kuna vitu vingi unajifunza kuhusu mafanikio, lakini kina unapojaribu kuviishi unashindwa. Labda umejifunza umuhimu wa kutumia muda wako vizuri na kutokuupoteza kwenye mambo yasiyo na tija. Unajaribu kuzingatia hilo ila bado unajikuta tu unapoteza muda kwa mambo yasiyo na tija. Labda umejifunza kwamba kuongea sana (more…)

#SheriaYaLeo (172/366); Onyesha udhaifu wako.

By | April 21, 2022

#SheriaYaLeo (172/366); Onyesha udhaifu wako. Jifunze kugeuza udhaifu wako kuwa njia ya kupata mamlaka. Pale unapoonekana imara na mkamilifu wakati wote, watu wanaweza kuona wewe siyo wa aina yao. Katika nyakati fulani unapaswa kuwaonyesha watu udhaifu wako ili waweze kuona wewe ni kama wao, na kukuamini zaidi. Hila linakufanya uwe (more…)

2667; Sumu ya mafanikio.

By | April 20, 2022

2667; Sumu ya mafanikio. Huwa kuna hadithi fupi kuhusu mwanzilishi wa Dubai ambayo huwa inazunguka sana mtandaoni. Mwanzilishi huyo anaulizwa anauonaje mustakabali wa nchi yake, anajibu kama ifuatavyo; Babu yangu aliendesha ngamia, baba yangu akaendesha ngamia, mimi ninaendesha Mercedea, mtoto wangu anaendesha Land Rover na mjukuu wangu atakuja kuendesha Land (more…)

#SheriaYaLeo (171/366); Wafanye wengine waje kwako.

By | April 20, 2022

#SheriaYaLeo (171/366); Wafanye wengine waje kwako. Pale unapoonekana kuwahitaji sana wengine na kwenda kuwafuata, unaishia kuonekana wa kawaida na hakuna anayekuthamini. Lakini pale unapowafanya watu waje kwako, kwa kuwa siyo rahisi wewe kupatikana, unakuwa wa tofauti na unathaminika. Kwa chochote unachofanya, wafanye watu waje kwako wakiwa na uhitaji. Wafanye waje (more…)

2666; Umetingwa na yapi?

By | April 19, 2022

2666; Umetingwa na yapi? Kutingwa au kuwa bize kama wengi walivyozoea kutumia ndiyo kuna nguvu kubwa ya kuamua matokeo ambayo mtu anayapata kwenye maisha yake. Kile kinachokuweka bize ndiyo kinachozalisha matokeo kwenye maisha yako. Matokeo unayopata sasa, iwe ni mazuri au mabaya yamezalishwa na yale yaliyokutinga huko nyuma. Usilaumu watu (more…)