Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (266/366); Wavuruge wasiweze kukusoma.

By | July 24, 2022

#SheriaYaLeo (266/366); Wavuruge wasiweze kukusoma. Nguvu ya maadui zako ipo kwenye uwezo wao wa kukusoma na kujua nia na mipango uliyonayo. Lengo la mikakati yako linapaswa kuwa ni kuwazuia maadui wasiweze kukusoma. Utaweza kukamilisha hilo kwa kuwavuruga maadui zako, kuwafanya wahangaike na mambo yasiyokuwa sahihi. Unachofanya ni kuigiza unafanya kitu (more…)

2761; Unajitofautishaje na wengine?

By | July 23, 2022

2761; Unajitofautishaje na wengine? Unajua ninj rafiki yangu, Neno siri za mafanikio limewanufaisha sana wengi. Kuna wengi ambao wameweza kuingiza kipato kikubwa kwa kuwaambia wengine kwamba wanazo siri za mafanikio. Sasa kwa sababu jamii kwa ujumla haiyaelewi mafanikio, hunasa kwenye huo mtego. Kwa kuamini kutakuwa na siri za mafanikio ndiyo (more…)

#SheriaYaLeo (265/366); Wafanye wakuambie siri zao.

By | July 23, 2022

#SheriaYaLeo (265/366); Wafanye wakuambie siri zao. Kwenye mchezo wa madaraka, lengo lako ni kuwa na udhibiti mkubwa wa matukio yajayo. Lakini tatizo kubwa litakalokukabili ni watu kutokuaa tayari kukuambia siri zao. Watu wanapokuwa na udhibiti kwenye kile wanachosema, huwa wanaficha yake maeneo muhimu au ambayo wana udhaifu mkubwa. Hilo linafanya (more…)

2760; Mipango haifanyiki uwanjani.

By | July 22, 2022

2760; Mipango haifanyiki uwanjani. Hebu fikiria timu ya mpira imeingia uwanjani kwa ajili ya mchezo wa fainali. Wakati mashabiki wanaishangilia timu hiyo na kutegemea makubwa, kocha ndiyo anawakusanya wachezaji na kuwauliza tutumie mbinu gani kushinda? Unajua kabisa timu ya aina hiyo itakuwa kwenye matatizo makubwa. Kwani wakati wa mapambano siyo (more…)

#SheriaYaLeo (264/366); Fanya tofauti na ulivyozoea.

By | July 22, 2022

#SheriaYaLeo (264/366); Fanya tofauti na ulivyozoea. Watu huwa wanategemea tabia zako zifanane na za watu wengine. Wajibu wako kama mwanamkakati bora ni kwenda kinyume na mazoea hayo. Washangaze watu kwa kufanya tofauti na vile ilivyozoelela. Kwa Sun Tzu na wanamikakati wengine, kufanya kitu cha tofauti bila ya utangulizi wa kitu (more…)

2759; Ninakuhitahu zaidi wakati una matatizo.

By | July 21, 2022

2759; Ninakuhitahu zaidi wakati una matatizo. Kitu kimoja ambacho nimeendelea kujifunza kwenye huduma ya ukocha ninayotoa ni pale ambapo watu wanaihitaji zaidi huduma yangu ndipo wanaikimbia. Pale mtu anapojikuta kwenye matatizo na changamoto kubwa, ndiyo unapaswa kuwa wakati mzuri kwake kutumia huduma ya ukocha kuvuka hilo. Lakini badala yake wengi (more…)

#SheriaYaLeo (263/366); Tumia wengine kukamilisha yasiyo mazuri.

By | July 21, 2022

#SheriaYaLeo (263/366); Tumia wengine kukamilisha yasiyo mazuri. Kama kuna mambo ambayo siyo mazuri yanapaswa kufanyika, hupaswi kuyafanya wewe mwenyewe, kwa sababu yataharibu sifa yako na kuwa kikwazo kwako. Badala yake unapaswa kuwatumia watu wengine kukamilisha mambo hayo. Kwa namna hiyo lawama zitaenda kwa watu hao wengine, huku wewe ukibaki na (more…)

#SheriaYaLeo (262/366); Mkakati wa hatua ndogo ndogo.

By | July 20, 2022

#SheriaYaLeo (262/366); Mkakati wa hatua ndogo ndogo. Tatizo kubwa ambalo watu wengi tunakabiliana nalo ni huwa tunakuwa na ndoto na matamanio makubwa. Ndoto hizo kubwa zinateka hisia zetu kiasi cha kujikuta tunashindwa kuangalia hatua ndogo tunazopaswa kuchukua ili kufikia ndoto hizo kubwa. Huwa tunapenda kufikiria hatua kubwa za kufikia ndoto (more…)

2757; Kuwepo na kutumika.

By | July 19, 2022

2757; Kuwepo na kutumika. Kinachowatofautisha wanaofanikiwa na wanaoshindwa siyo kuwepo au kutokuwepo kwa vitu fulani, bali kutumika au kutokutumika kwa vitu hivyo. Kwa mfano wale waliofanikiwa huwa wanatumia uwezo mkubwa ulio ndani yao. Hiyo haimaanishi kwamba wanaoshindwa hawana uwezo mkubwa ndani yao. Wanao sana, ila kinachowakwamisha ni kutokuutumia. Na mara (more…)