Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (236/366); Jua na tumia udhaifu wa watu.

By | June 24, 2022

#SheriaYaLeo (236/366); Jua na tumia udhaifu wa watu. Sisi binadamu huwa tuna upinzani. Huwa hatupendi kupangiwa nini tufanye na nini tusifanye. Tunapenda kuona tukifanya maamuzi yetu wenyewe. Huwa tunapinga na kukataa mabadiliko yoyote tunayopendekezewa na wengine. Katika kuwashawishi watu, kukabiliana nao kwenye upinzani wao huwa siyo njia sahihi. Utatumia nguvu (more…)

2731; Fanya kazi kwa juhudi na utafanikiwa.

By | June 23, 2022

2731; Fanya kazi kwa juhudi na utafanikiwa. Ipo nukuu moja ya Kiingereza ambayo ilikuwa ikitumiwa na moja ya familia tajiri sana dunian. Nukuu hiyo kwa Kiingereza inasema; Work hard and you will succeed. Ikimaanisha; Fanya kazi kwa juhudi na utafanikiwa. Iko wazi na inaeleweka kabisa, kwamba ukifanya kazi kwa juhudi, (more…)

#SheriaYaLeo (235/366); Wape ambacho hawajakizoea.

By | June 23, 2022

#SheriaYaLeo (235/366); Wape ambacho hawajakizoea. Ni asili yetu binadamu kupenda kile ambacho hatuna. Huwa tunaona maisha ya wengine ni bora kuliko yetu pale wanapokuwa na vitu ambavyo sisi hatuna. Huwa tunaona kazi au biashara za wengine ni nzuri kuliko zetu. Tunaona maisha yao ni mazuri kuliko yetu. Mara zote tunatamani (more…)

2730; Sumu inayoua taratibu.

By | June 22, 2022

2730; Sumu inayoua taratibu. Nikikuambia sasa hivi unywe sumu ambayo itakatisha maisha yako mara moja utanishangaa sana. Utaniambia huwezi kufanya hivyo, kwa sababu bado unataka kuishi. Lakini tukikuchunguza kwa kina, kwa namna unavyofanya mambo yako, tunaweza kuona huna tofauti sana na anayetumia sumu. Tofauti pekee ni sumu unayotumia wewe inaua (more…)

#SheriaYaLeo (234/366); Mhamasishaji mkuu.

By | June 22, 2022

#SheriaYaLeo (234/366); Mhamasishaji mkuu. Watu wengi huwa wanapenda kuhamasisha kwa kutumia maneno. Lakini maneno pekee huwa hayana nguvu ya ushawishi. Na pia huwa yanasahaulika haraka. Kama unataka kuwa na ushawishi mkubwa kwa wengine, kuna mambo mawili muhimu unapaswa kuyazingatia. La kwanza ni kuonyesha kwa vitendo. Watu wanaelewa, kuhamasika na kukumbuka (more…)

#SheriaYaLeo (233/366); Jinsi ya kuwakabili wasumbufu.

By | June 21, 2022

#SheriaYaLeo (233/366); Jinsi ya kuwakabili wasumbufu. Kwenye maisha utakutana na watu wasumbufu. Watu ambao kwa kuwa wana uwezo mkubwa kuliko wengine, huona kama hawahitaji kufuata taratibu wanazozifuata wengine. Watu hao hufanya tofauti na wanavyofanya wengine na wanapoulizwa huomba radhi na kuahidi kufanya kwa usahihi. Lakini bado wakati mwingine hawafanyi kwa (more…)

2728; Ni wewe umewafundisha.

By | June 20, 2022

2728; Ni wewe umewafundisha. Kwa namna yoyote ile ambayo watu wanakuchukulia, ni wewe mwenyewe umewafundisha wakuchukulie hivyo. Umewapa ruhusa kwamba wanaweza kukuchukulia kwa namna wanavyokuchukulia. Kama watu wanakudharau maana yake umewafundisha wakudharau. Kuna namna umejiweka ambayo inawafanya watu waone ni sawa kukudharau. Kadhalika kama watu wanakuheshimu maana yake umewafundisha hivyo. (more…)

#SheriaYaLeo (232/366); Wape ushindi kwenye mambo madogo.

By | June 20, 2022

#SheriaYaLeo (232/366); Wape ushindi kwenye mambo madogo. Kama unataka kuwashawishi watu wakubaliane na wewe kwenye jambo kubwa unalotaka, wape kwanza ushindi kwenye mambo madogo. Angalia mambo madogo ambayo hayana athari kwenye lile kubwa unalotaka, kisha kubaliana nao kwenye mambo hayo. Katika kukubaliana nao kwenye mambo hayo madogo unakuwa umewaweka kwenye (more…)

2727; Tengeneza wasiwasi wenye manufaa.

By | June 19, 2022

2727; Tengeneza wasiwasi wenye manufaa. Sisi binadamu mara zote huwa tunakuwa na wasiwasi. Hata kama mambo yako sawa kabisa, huwa hatukosi kitu kinachotupa wasiwasi. Tena pale mambo yanapokuwa sawa ndiyo tunakuwa na wasiwasi mkubwa zaidi. Tukifikiria vipi mambo hayo yakiharibika. Hata kama hakuna tatizo lolote, huwa tunatengeneza matatizo ya kufikirika (more…)