Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (176/366); Tumia maneno matupu.

By | April 25, 2022

#SheriaYaLeo (176/366); Tumia maneno matupu. Watu huwa wanapenda na hata kuelewa zaidi lugha ya picha. Hiyo ni kwa sababu inawawezesha kujenga taswira ya kitu na kukielewa vizuri. Unapotaka kuwahadaa watu, nenda kinyume na hilo. Tumia lugha ya maneno matupu ambayo hayamwezeshi mtu kujenga taswira yoyote. Lugha ya aina hiyo inamfanya (more…)

2671; Wana ndoto, wasaidie wazifikie.

By | April 24, 2022

2671; Wana ndoto, wasaidie wazifikie. Falsafa kuu ya KISIMA CHA MAARIFA ni unawesa kupata chochote unachotaka kama utawasaidia wengi zaidi kupata kile wanachotaka. Ndiyo, kuna vitu tunavitaka, ila kuvipata ni mpaka kwanza tuwasaidie wengine kupata vile wanavyotaka. Kila mtu hapa duniani ana ndoto mbalimbali anazotaka kuzifikia. Kwenye kila eneo la (more…)

#SheriaYaLeo (175/366); Jinsi ya kuwafanya watu wawe tayari kukusaidia.

By | April 24, 2022

#SheriaYaLeo (175/366); Jinsi ya kuwafanya watu wawe tayari kukusaidia. Kama unataka watu wakusaidie kitu fulani, usiwakumbushe jinsi ambavyo wewe umewahi kuwasaidia huko nyuma. Unaweza kudhani kwa kuwakumbusha hilo wataona wanapaswa kulipa fadhila na hivyo kusukumwa kukusaidia. Lakini siyo kinachotokea. Unapowakumbusha watu jinsi ulivyowasaidia huko nyuma unawafanya wajione hawajiwezi na wanategemea (more…)

#SheriaYaLeo (174/366); Dhibiti kile unachosema.

By | April 23, 2022

#SheriaYaLeo (174/366); Dhibiti kile unachosema. Mamlaka ni mchezo wa mwonekano kadiri unavyozungumza kidogo, ndivyo unavyoonekana wa muhimu na mwenye mamlaka makubwa. Unapokaa kimya unawafanya wengine washindwe kukutabiri. Maana sisi binadamu ni mashine za kutengeneza maana, huwa hatuwezi kutulia kama hatujui maana au nia ya kitu fulani. Unapozungumza sana, unaweka kila (more…)

2669; Nini ni sahihi na siyo nani yuko sahihi.

By | April 22, 2022

2669; Nini ni sahihi na siyo nani yuko sahihi. Changamoto kubwa tunazokutana nazo kwenye maisha huwa zinaanzia kwenye hukumu tunazotoa kwa wengine. Mara nyingi hukumu hizo huwa ni za upendeleo. Kama mtu tunampenda au kukubaliana naye tunamhukumu vizuri kwa sababu tunaona upande wake mzuri tu. Na kama mtu hatumpendi au (more…)

#SheriaYaLeo (173/366); Chukua mamlaka tararibu.

By | April 22, 2022

#SheriaYaLeo (173/366); Chukua mamlaka tararibu. Ukionekana una haraka sana ya kuchukua mamlaka, utaishia kuibua hasira, wivu na chuki. Watu hawatakuwa tayari kukuachia uchukue mamlaka kwa vile unavyotaka. Hivyo njia bora ni kuchukua mamlaka hayo taratibu. Kujipa muda wa kutosha katika kukamilisha hilo. Kwanza wape watu nafasi ya kuona wanafanya kwa (more…)

2668; Haya mambo huwezi kuyalazimisha.

By | April 21, 2022

2668; Haya mambo huwezi kuyalazimisha. Kuna vitu vingi unajifunza kuhusu mafanikio, lakini kina unapojaribu kuviishi unashindwa. Labda umejifunza umuhimu wa kutumia muda wako vizuri na kutokuupoteza kwenye mambo yasiyo na tija. Unajaribu kuzingatia hilo ila bado unajikuta tu unapoteza muda kwa mambo yasiyo na tija. Labda umejifunza kwamba kuongea sana (more…)

#SheriaYaLeo (172/366); Onyesha udhaifu wako.

By | April 21, 2022

#SheriaYaLeo (172/366); Onyesha udhaifu wako. Jifunze kugeuza udhaifu wako kuwa njia ya kupata mamlaka. Pale unapoonekana imara na mkamilifu wakati wote, watu wanaweza kuona wewe siyo wa aina yao. Katika nyakati fulani unapaswa kuwaonyesha watu udhaifu wako ili waweze kuona wewe ni kama wao, na kukuamini zaidi. Hila linakufanya uwe (more…)

2667; Sumu ya mafanikio.

By | April 20, 2022

2667; Sumu ya mafanikio. Huwa kuna hadithi fupi kuhusu mwanzilishi wa Dubai ambayo huwa inazunguka sana mtandaoni. Mwanzilishi huyo anaulizwa anauonaje mustakabali wa nchi yake, anajibu kama ifuatavyo; Babu yangu aliendesha ngamia, baba yangu akaendesha ngamia, mimi ninaendesha Mercedea, mtoto wangu anaendesha Land Rover na mjukuu wangu atakuja kuendesha Land (more…)