Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (162/366); Waambukize watu hisia chanya.

By | April 11, 2022

#SheriaYaLeo (162/366); Waambukize watu hisia chanya. Sisi binadamu ni viumbe wa kihisia. Unapokuwa ndani ya kundi lolote lile, hasa kama kiongozi, waambukize watu hisia chanya kwa kuwapa hamasa ya kuweza kufanya makubwa zaidi. Washirikishe maono makubwa na malengo ya kufika kwenye maono hayo. Waonyeshe ung’ang’anizi katika kufikia maono hayo. Pia (more…)

2657; Huo mpango wako umekufikisha wapi?

By | April 10, 2022

2657; Huo mpango wako umekufikisha wapi? Hatua ya kwanza kabisa katika kupata matokeo makubwa na ya tofauti ni kuwa na mpango tofauti. Kufanya kile ambacho umekuwa unafanya, utaendelea kupata matokeo unayoyapata sasa. Kile ambacho kimekufikisha hapo ulipo sasa, kitakubakisha hapo hapo. Kama unataka kwenda zaidi ya hapo ulipo sasa, lazima (more…)

#SheriaYaLeo (161/366); Wafanye watu wajisikie wako juu.

By | April 10, 2022

#SheriaYaLeo (161/366); Wafanye watu wajisikie wako juu. Watu wanapenda sifa na kutukuzwa, wanapenda kuona wapo juu na wengine wanawategemea kwa mambo mbalimbali. Pale unapotaka kitu kutoka kwa watu, hasa wale wenye mamlaka, wafanye wajione wako juu. Wafanye waone upo chini yao na unawategemea sana kwa kile unachotaka. Hilo linawafanya wajione (more…)

2656; Teknolojia itakunyoosha.

By | April 9, 2022

2656; Teknolojia itakunyoosha. Siku siyo nyingi nilikuwa nataka kuwahi mahali na hivyo kuhitaji usafiri wa haraka wa pikipiki. Nikitumia mtandao wa kuita vyombo vya usafiri na mara moja usafiri ukaja. Lakini dereva aliyekuja hakuwa mzuri, hakuendesha vizuri wala kufuata vyema maelekezo. Pamoja na kumwambia lakini hakuonekana kusikiliza au kuelewa. Basi (more…)

#SheriaYaLeo (160/366); Wavuruge wasijue nia yako halisi.

By | April 9, 2022

#SheriaYaLeo (160/366); Wavuruge wasijue nia yako halisi. Kwa chochote unachotaka, kuna watu ambao ni kikwazo kwako, ambao wapo tayari kukuzuia usikipate. Njia bora ya kuwavuka watu hao na kupata kile unachotaka ni kuwavuruga. Unawavuruga kwa kuwahadaa, kuwafanya waone unataka kitu kingine ambacho siyo nia yako halisi. Kwa njia hii huendei (more…)

2655; Tatizo lako umekosa msimamo.

By | April 8, 2022

2655; Tatizo lako umekosa msimamo. Unakumbuka ile siku ambayo ulihudhuria semina, ukajifunza mambo mengi na kutoka na hamasa ya kwenda kuyabadili kabisa maisha yako. Siku chache za mwanzo ukawa wa tofauti kabisa, ukijituma kweli kweli. Lakini baada ya muda ukarudi kwenye mazoea yako. Unakumbuka mara zote ambazo umekuwa unasoma vitabu (more…)

#SheriaYaLeo (159/366); Usidharau akili za wengine.

By | April 8, 2022

#SheriaYaLeo (159/366); Usidharau akili za wengine. Huwa hatupendi kukubali kwamba wengine wana akili kuliko sisi. Tunapokutana na watu wenye akili sana, huwa tunatafuta kila njia ya kujitetea ili kuonyesha kwamba hatupo nyuma. Tutasema wana akili za darasani tu. Au wana akili kwa sababu walisoma shule za gharama kubwa. Au wana (more…)

2654; Kumbuka wewe ni binadamu.

By | April 7, 2022

2654; Kumbuka wewe ni binadamu. Kadiri ninavyokaa kwenye hii huduma ya ukocha, ndivyo ninavyojifunza kwa karibu tabia za watu na kuwa bora zaidi katika kuwasaidia kufika kule wanakotaja kufika. Zamani alikuwa akija mtu kwangu, mwenye njaa kweli ya mafanikio na anayesema yupo tayari kufanya kazi usiku na mchana ili kupata (more…)

#SheriaYaLeo (158/366); Igiza nafasi yako vizuri.

By | April 7, 2022

#SheriaYaLeo (158/366); Igiza nafasi yako vizuri. Maisha ni maigizo, kile ambacho watu wanaonyesha kwa nje, sivyo walivyo ndani yao. Hivyo moja ya wajibu wako mkubwa kwenye maisha ni kuigiza nafasi yako vizuri. Hasa kwenye eneo la hisia, lazima uweze kuvaa hisia sahihi kwa wakati sahihi. Pale unapohitajika kuwa na hisia (more…)