Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (166/366); Kuwa mkali.

By | April 15, 2022

#SheriaYaLeo (166/366); Kuwa mkali. Mara nyingi huwa tunapenda kuwa wapole na wenye kujali wengine ili kuweza kuendana nao vizuri na kupata kile tunachotaka. Hili huwa linafanya kazi vizuri wakati wa kawaida. Lakini wakati wa hatari hilo linakuwa mzigo kwako, kufanya hivyo kunapelekea watu wakuone ni mtu unayefaa kuonewa, kukatishwa tamaa (more…)

2661; Wanakuvuruga usione uhalisia.

By | April 14, 2022

2661; Wanakuvuruga usione uhalisia. Mpishi mmoja mbobezi amewahi kusema njia ya haraka ya kujua kama chakula ni kizuri au kibaya ni kuangalia viungo ambavyo vimewekwa kwenye chakula hicho. Akaendelea kusema unapoona chakula kina viungo vingi sana, jua siyo kizuri. Hivyo wanaweka viungo vingi ili kukuvuruga usione uhalisia. Alitumia maneno makali (more…)

#SheriaYaLeo (165/366); Ongoza ukiwa mbele.

By | April 14, 2022

#SheriaYaLeo (165/366); Ongoza ukiwa mbele. Unapokuwa kiongozi, unahitaji kuwa na ushawishi mkubwa kwa wale unaowaongoza ili wafanye yale wanayopaswa kufanyika. Huwezi kupata ushawishi huo kwa kulazimisha au kubembeleza. Hizo ni njia zenye matokeo ya muda mfupi ila siyo endelevu. Njia bora ya kuwa na ushawishi kwa wale unaowaongoza ni kuwa (more…)

2660; Huwezi kuhangaika na kila kitu.

By | April 13, 2022

2660; Huwezi kuhangaika na kila kitu. Kwenye kila tasnia, mabadiliko na matokeo makubwa huwa yanazalishwa na vijana. Lakini cha kushangaza vijana hao hao wakishafikia mafanikio makubwa kwenye tasnia zao na kuwa watu wazima, wanaacha kufanya makubwa. Hapa napenda tujifunze kitu kikubwa sana ambacho tunaweza kukitumia kwenye kila umri na kikatusaidia (more…)

#SheriaYaLeo (164/366); Tumia mbinu ya kujisalimisha.

By | April 13, 2022

#SheriaYaLeo (164/366); Tumia mbinu ya kujisalimisha. Unapokuwa dhaifu, usipambane na mwenye nguvu. Badala yake chagua kujisalimisha. Kupambana na mwenye nguvu huku wewe ukiwa dhaifu ni kuchagua kushindwa vibaya. Kujisalimisha kunakupa nafasi ya kujipanga na kukusanya nguvu zako ili baadaye uweze kushambulia na kushinda. Kujisalimisha kunamfanya adui yako akudharau na kukuona (more…)

2659; Tafuta changamoto zaidi.

By | April 12, 2022

2659; Tafuta changamoto zaidi. Watu wengi hufikiri maisha yasingekuwa na changamoto ndiyo yangekuwa mazuri na yenye furaha. Lakini ukweli ni kwamba maisha hayatakuja kukosa changamoto. Kila wakati maisha yatakuwa na changamoto fulani. Hata ukishakuwa na kila unachokitaka, ukawa na uhuru kamili wa kifedha, bado changamoto zitakuwepo tu. Hata kama huhitaji (more…)

#SheriaYaLeo (163/366); Mwondoe mwenye ushawishi.

By | April 12, 2022

#SheriaYaLeo (163/366); Mwondoe mwenye ushawishi. Kwenye kundi lolote lile huwa kuna mtu mmoja mwenye ushawishi mkubwa na ambaye wengine wote wanamsikiliza. Na hata kunapokuwa na matatizo, chanzo chake kikuu huwa ni mtu mmoja mwenye ushawishi. Pale anapokuwa hajaridhika kwa namna fulani anakuwa tayari kusambaza hilo kwa wengine na kuwa chanzo (more…)

MWONGO WA KUFIKIA UBILIONEA (2020 – 2030).

By | April 11, 2022

MWONGO WA KUFIKIA UBILIONEA (2020 – 2030). Muongo wa 2020 – 2030 ni muongo wa kufikia kiwango cha utajiri cha UBILIONEA kwenye KISIMA CHA MAARIFA. Hiki ni kipindi ambacho kila mwanachama anapaswa kufikia uhuru wa kifedha kwenye maisha yake. Ni kupitia uhuru huo wa kifedha ndipo kila mwanachama anaweza kuwa (more…)

Ongea Na Kocha; Kuongeza Kiwango Cha Faida, Mwongozo Wa Kufika Kwenye Ubilionea.

By | April 11, 2022

Habari mwanamafanikio? Karibu kwenye kipindi cha ONGEA NA KOCHA ambacho kina mambo mawili makubwa. Jambo la kwanza ni mjadala wa sehemu ya mwisho ya kitabu cha INSTANT CASHFLOW inayohusu kuongeza kiwango cha faida. Wanamafanikio wameshirikisha njia tano walizochagua kufanyia kazi kwenye biashara zao ili kuweza kuongeza kiwango cha faida. Ni (more…)

2658; Inalipa sana.

By | April 11, 2022

2658; Inalipa sana. Huu ndiyo mtego ambao umewanasa na kuwapoteza wengi kuliko kitu kingine chochote. Kwa kuwa watu wana tamaa ya pesa, tena zinazoweza kupatikana kirahisi bila ya kufanya kazi yoyote, mtego huu umewanasa wengi mno. Mtu anaposikia kitu fulani kinalipa sana, anaona hicho ndiyo cha kufanya maana anachoangalia yeye (more…)