Category Archives: BIASHARA NA UJASIRIAMALI

BIASHARA LEO; Kabla Ya Mteja Kununua Unachouza, Anakununua Wewe Kwanza.

By | April 12, 2016

Biashara inaonekana rahisi pale unapofikiria kununua na kuuza pekee. Au kuandaa bidhaa au huduma yako kisha kusubiri wateja waje wa nunue. Lakini biashara siyo rahisi hivi, na ndio maana wengi wanashindwa. Kwa sababu huwa wanafikiri ukishakuwa na mtaji tu unaendesha biashara. Kinachoongeza ugumu kwenye biashara ni ile hali kwamba wateja (more…)

Ujasiriamali Kupitia Mtandao Wa Intaneti.

By | April 11, 2016

Kama umeweza kusoma hapa, nina uhakika kwamba unajua nini maana ya mtandao wa intaneti. Moja ya mapinduzi makubwa sana ambayo tunayapitia katika zama hizi ni uwepo wa mtandao wa intaneti. Mtandao huu umeleta mabadiliko makubwa sana kwenye kila eneo la maisha yetu. Mtandao wa intaneti umerahisisha njia za mawasiliano, umerahisisha (more…)

BIASHARA LEO; Makadirio Ya Matumizi Na Faida.

By | April 7, 2016

Unapoweka mipango yako ya kibiashara, ni lazima uwe na makadirio. Na linapokuja swala la fedha kuna makadirio mengi ambayo huwa tunayafanya kama wafanyabiashara. Tunakadiria matumizi yetu ya kibiashara, na pia tunakadiria mapato yetu na faida pia. Kitu kimoja cha kushangaza sana kuhusu makadirio yetu ni kwamba huwa siyo sahihi, karibu (more…)

BIASHARA LEO; Usitumie Biashara Mpya Kuua Biashara Yako Ya Zamani.

By | April 5, 2016

Unapoanza na biashara moja na ukaona inafanya vizuri, unapata mawazo ya kukua zaidi kibiashara, na kufikiria kufungua biashara nyingine mpya. Hili ni wazo zuri sana kwa sababu huwezi kubaki pale pale kwa siku zote, kama mfanyabiashara makini ni lazima ukue. Lakini hapa kwenye ukuaji, hasa wa kuanzisha biashara mpya kuna (more…)

Tengeneza mfumo bora wa wafanyakazi kwenye biashara yako.

By | April 4, 2016

Kama unaendesha biashara ndogo ambayo unategemea siku moja ikue, basi jambo kubwa la kuzingatia kuanzia sasa ni kutengeneza mfumo bora wa wafanyakazi kwenye biashara yako. na kama tayari biashara yako ni kubwa, unahitaji kuwa na mfumo bora wa ufanyaji kazi kwenye biashara yako. Jambo hili ni muhimu kwa sababu wafanyabiashara (more…)

BIASHARA LEO; Unachojifunza Kutoka Biashara Za Wengine.

By | April 1, 2016

Pamoja na kwamba wewe ni mfanyabiashara, bado pia wewe ni mteja kwenye biashara za wengine. Ukianzia na unapopata mahitaji yako muhimu na hata unapopata huduma nyingine muhimu kwako. Usiishie tu kuwa mteja, bali hakikisha kupitia uteja wako unajifunza mbinu za kuboresha biashara yako. Kila unapokwenda kununua kwenye biashara nyingine, jiulize (more…)

BIASHARA LEO; Njia Rahisi Ya Kuua Biashara Yako.

By | March 30, 2016

Kuna njia nyingi sana unazoweza kutumia kuua biashara yako. Kwanza elewa kwamba wewe mwenyewe ndiye utakayeua biashara yako. Siyo mtu mwingine yeyote, ni wewe kwa kufanya au kutokufanya mambo fulani kwenye biashara yako. Sasa turudi kwenye hiki tulichopanga kujadili leo. Njia rahisi sana ya kuua biashara yako ni kuacha kujali (more…)

Kitu muhimu kwa mteja wako kuliko fedha anayokupa.

By | March 28, 2016

Mara nyingi wafanyabiashara tumekuwa tukijiuliza iwapo bidhaa au huduma tunayomuuzia mteja wetu inaendana na thamani ya fedha anayotoa. Kwa njia hii tumekuwa tunachukulia fedha ya mteja kama ndiyo kitu muhimu sana kwao, na hivyo kuhakikisha hawapotezi fedha zao kwa kufanya biashara na sisi. Ni kweli kabisa fedha ya mteja ni (more…)

BIASHARA LEO; Viashiria Kwamba Umeshaingia Kwenye Ushindani Utakaokupoteza Kibiashara.

By | March 25, 2016

Kama ambavyo nimekuwa nasisitiza mara nyingi, ushindani wa moja kwa moja kwenye biashara, ndiyo mchezo mbaya kuliko yote unaoweza kufanya kwenye biashara yako, kwa sababu utakupoteza haraka sana. Mfanyabiashara mwenzetu aliandika maoni kutaka kujua ni viashiria gani mfanyabiashara anaweza kuwa navyo pale anapokuwa ameingia kwenye mashindano ya kibiashara.Aliandika maoni yake (more…)

BIASHARA LEO; Kitu Kimoja Unachoweza Kumpoteza Nacho Mshindani Wako Wa Biashara.

By | March 23, 2016

Kama ambavyo nimekuwa nakuambia mara nyingi, kwenye biashara usiingie kwenye mashindano ya moja kwa moja na washindani wako, maana hii itakuumiza zaidi ya kukujenga. Unapoingia kwenye mashindano ya moja kwa moja, mshindani wako anaweza kufanya jambo lolote ambalo linaweza kuwaathiri wote wawili kwenye biashara zenu. Lakini pia nimekuwa nakushirikisha mbinu (more…)