Category Archives: BIASHARA NA UJASIRIAMALI

BIASHARA LEO; Pale Unaposikia “BIASHARA FULANI INALIPA SANA” Jua Umeshachelewa.

By | April 23, 2015

Kuna baadhi ya biashara huwa zinakwenda na misimu fulani. Kuna kipindi watu wanakuwa wanazungumzia sana biashara ya aina fulani, inapata umaarufu sana na kila mtu anakimbilia kuifanya. Hizi ni zile hadithi kwamba biashara fulani inalipa sana, ona watu fulani wamefanya na wamepata faida kubwa. Au kilimo fulani kinalipa sana, ona (more…)

BIASHARA LEO; Usimseme Vibaya Mshindani Wako Mbele Ya Mteja Wako.

By | April 22, 2015

KARIBU KWENYE SEMINA YA MAFANIKIO KUPITIA BIASHARA MWAKA 2015. AMKA CONSULTANTS imekuandalia semina ya mafanikio kwenye biashara mwaka 2015. Katika semina hii utajifunz amambo yote muhimu yatakayokuwezesha kuanza, kukuza na kufikia mafanikio kwenye biashara yako. Semina itaanza tarehe 04/05/2015 na itaendeshwa kwa mwezi mzima kwa njia ya mtandao(yaani email). Mwisho (more…)

BIASHARA LEO; Njia TANO Rahisi Za Kutangaza Biashara Yako.

By | April 21, 2015

Hata uwe na bidhaa au huduma bora kiasi gani, kama watu hawajui ipo, huna biashara. Jukumu lako kubwa kwenye biashara ni kuweza kulifikia soko lako. Kila mwenye uhitaji ajue hitaji lake linaweza kutatuliwa wapi. Njia ya uhakika ya kulifikia soko lako ni kupitia matangazo. Katika matangazo mteja anajua kwmaba upo (more…)

Karibu Kwenye Semina Ya Mafanikio Kwenye Biashara Mwaka 2015.

By | April 20, 2015

Huu ni wakati ambao karibu kila mtu anahitaji kuingia kwenye biashara. Haijalishi mtu ameajiriwa au hana ajira, haijalishi kiwango cha elimu mtu alichonacho na wala haijalishi umri wa mtu, kwa sasa kila mtu anahitaji kuwa kwenye biashara. Ajira zimekuwa za shida kupatikana na hata wale wanaozipata bado haziwawezeshi kuyamudu maisha. (more…)

Hivi ndivyo unavyoweza kuwahamasisha wafanyakazi wako ili wawe na uzalishaji mkubwa.

By | April 20, 2015

Katika makala mbili zilizopita tumekuwa tunajadili kuhusu mteja muhimu na wa kwanza kwenye biashara yako. Tuliona mteja huyu ni mfanyakazi au wafanyakazi wako uliowaajiri kwenye biashara yako. Hawa ni watu ambao wanatakiwa kuwa washabiki wa kwanza kabisa wa kile amabcho unafanya. Wanatakiwa kuwa wanakipenda na wapo tayari kuwashawishi wengine wajihusishe (more…)

BIASHARA LEO; Hawa Ndio Wateja Rahisi Kuwapata Kwenye Biashara Yako.

By | April 18, 2015

Moja ya changamoto ambazo zinawazuia wafanyabiashara wengi kufikia mafanikio ni upatikanaji wa wateja. Wafanyabiashara wengi sana hutumia nguvu nyingi kumfanya mteja afike kwenye biashara yake, lakini mteja anapofika pale anajilaumu ni kitu gani kimempeleka pale na hatokuwa tayari kurudi tena. SOMA; Maswali Matatu Muhimu Ya Kujiuliza Kwenye Wazo Lako La (more…)

BIASHARA LEO; Tumia Sheria Ya Mara 2, Mara 3 Kwenye Mipango Yako Ya Biashara.

By | April 17, 2015

Pamoja na uwezo mkubwa ambao tunao, pamoja na maarifa mengi tunayoweza kujikusanyia bado hakuna mtu anayeweza kuitabiri kesho kwa asilimia 100. Hakuna. Hakuna anayejua ni nini kitakachotokea kesho kwenye maisha yake au biashara yake. Lakini hii haituzii kuweka na kufanyia kazi mipango yetu kwenye maisha na biashara zetu. SOMA; Unapokuwa (more…)

BIASHARA LEO; Mteja Hajui Anachotaka, Ila Anajua Kitu Hiki Muhimu Sana.

By | April 16, 2015

Kama unataka kukuza biashara yako na ifikie viwango vya juu sana basi usitegemee sana maoni ya wateja, hasa kuhusu ni nini wanataka. Ukiondoa biashara za uchuuzi ambazo mtu anakwenda dukani moja kwa moja kununua sukari, biashara nyingi mteja hajui anachotaka. Ndio hajui ni kitu gani hasa anachokitaka, ila akikipata atafurahia (more…)

BIASHARA LEO; Usitupigie Kelele, Tupe Sababu.

By | April 15, 2015

Ndio akili ya mteja inavyowaza hivi hata kama hakuambii. Biashara za kupiga kelele sasa hivi zimeshapitwa na wakati. Hizi ni zama za biashara za kutoa sababu. Tuambie kwa nini tufanye biashara na wewe. Kupiga kelele. Kupiga kelele ni pale ambapo unatumia nguvu nyingi kutangaza biashara yako, ila unashindwa kujenga mahusiano (more…)

BIASHARA LEO; Kitu Muhimu Kujua Kuhusu Mteja Wako.

By | April 14, 2015

Mafanikio yako kwenye biashara yanategemea kwa kiasi kikubwa ni jinsi gani unamjua mteja wako vizuri. Kumbuka tulishakubaliana kwamba lengo lako kubwa kwenye biashara ni kutengeneza wateja na ukishaliweza hilo faida inafuata bila hata ya kuumiza sana kichwa. Nasisitiza sana hili la wateja kwa sababu ndipo udhaifu mkubwa ulipo kwa wafanyabiashara (more…)