Category Archives: BIASHARA NA UJASIRIAMALI

BIASHARA LEO; Fanya Kitu Hiki Kimoja Tu, Achana Na Vingine Vyote.

By | April 13, 2015

Kuna kitu kimoja ukikifanya kwenye biashara yako, utaleta mabadiliko makubwa sana. Utaikuza biashara yako na mambo mengine yote yatakwenda vizuri. Kwa kufanya kitu hiki kimoja na ukakifanya vizuri unajiweka wkenye nafasi ya kuweza kufikia mafanikio makubwa sana hata kama biashara unayofanya ina ushindani mkubwa. SOMA; Hiki Ndio Unachotakiwa Kufanya. Je (more…)

Mambo muhimu ya kuzingatia wakati unaajiri kwenye biashara yako.

By | April 13, 2015

Katika makala ya wiki iliyopita tuliona mteja wa kwanza na wa muhimu sana kwenye biashara yako. Tulijifunza kwmaba mteja huyu ni muhimu sana na ndiye wa kwanza kuridhishwa kabla hata mteja mwingine hajafika kwenye biashara yako. Mteja huyu ni mfanyakazi wako au msaidizi katika biashara yako. Tuliona kwamba msaidizi yeyote (more…)

BIASHARA LEO; Mafanikio Ya Biashara Yanaanza Na Wewe Mwenyewe.

By | April 11, 2015

Nimekuwa napata bahati ya kukutana na kuwasiliana na wafanyabiashara wengi wadogo na wa kati kwa ajili ya ushauri. Kitu kikubwa ambacho nimekuwa nakiona ni mtazamo wa mtu kwenye biashara una athari kubwa sana kwenye biashara ya mtu. Kuna watu ambao wanafanya biashara kwa sababu wanataka tu kupata faida. Hawa ni (more…)

BIASHARA LEO; Biashara Yako Ni Matatizo Ya Watu…

By | April 10, 2015

Mbinu bora kabisa itakayokuwezesha wewe kufanya biashara yako wka mafanikio ni kubadili mtazamo wako katika biashara unayofanya. Tulishakubaliana kwamba lengo la biashara sio kupata faida bali kutengeneza wateja wa kudumu, kama tulivyoona hapa; Lengo La Biashara Sio Kupata Faida, Bali Ni Hili Hapa. Sasa leo tutajifunza mbinu nyingine muhimu ambayo (more…)

BIASHARA LEO; Kama Unabadili Bei Kamwe Usifanye Hivi…

By | April 9, 2015

Kama umekuwa mfuatiliaji mzuri wa mafunzo ninayotoa utakuwa unaelewa kwamba tunajaribu kujenga utamaduni mpya kwenye biashara. Na utamaduni huu ni ule wa kufanya biashara kirafiki na kuwa na wateja ambao wanakuamini na kukutegemea. Mbinu nyingi tunazoshirikishana ni za kuweza kumfanya mteja awe rafiki yako na afurahie kufanya biashara na wewe. (more…)

BIASHARA LEO; Faida Ya Kushindwa Kwenye Biashara.

By | April 8, 2015

Kama utajifunza biashara kabla ya kuingia kwenye biashara utajifunza vitu vingi sana. Utajua kila aina ya kanuni na kila aina ya mbinu ya kuanza na kukuza biashara yako. Lakini unapoingia kwenye biashara yenyewe mambo hayaendi kiulaini kama ulivyokuwa unajifunza. Kwenye biashara halisi sio kwmaba kila kitu kitakwenda kama ulivyokuwa umepanga (more…)

BIASHARA LEO; Ingia Kwenye Biashara Yenye Ushindani Lakini Usishindane.

By | April 7, 2015

Moja ya faida za kuingia kwenye biashara katika kipindi hiki ni kwmaba huna haja ya kuumiza sana kichwa ni biashara gani ufanye. Japo wengi bado wanaumia vichwa. Zama hizi kila aina ya biashara inafanywa, tena kama unapanga kuingia kwenye biashara ndogo ndogo basi popote ulipo kuna biashara zaidi ya 100 (more…)

BIASHARA LEO; Tumia Kigezo Hiki Katika Bei Ili Uweze Kufanikiwa.

By | April 6, 2015

Ni kigezo gani ambacho unatumia kupanga bei ya bidhaa au huduma zako? Je unaangalia watu wanaweza kumudu? Je unaangalia ni bei ipi itakuletea wateja wengi? Je unaangalia wengine wameweka bei gani? Vigezo vyote hivyo unawez akuvitumia ila kuna kigezo kimoja muhimu sana ambacho wengi, hasa wafanyabiashara wadogo hawakitumii. Kigezo hiki (more…)

Mteja wa kwanza na wa muhimu sana kwenye biashara yako.

By | April 6, 2015

Katika moja ya makala zilizopita hapa kwenye KONA YA MJASIRIAMALI tuliwahi kujadili lengo kuu la biashara ni nini. Kama hukumbuki au hukupata nafasi ya kusoma makala ile tuliona kwamba lengo kuu la biashara sio kupata faida kama watu wengi wanavyofikiria. Bali lengo kuu la biashara ni kutengeneza wateja. Kama biashara (more…)

BIASHARA LEO; Kwa Nini Watu Hawawaambii Wengine Kuhusu Biashara Yako.

By | April 4, 2015

Njia bora kabisa ya kutangaza biashara yako ni kushawishi mtu anayenunua kwako au mteja wako kuwaambia wengine kuhusu biashara yako. Yaani mteja wako anapata huduma au bidhaa kwako na anapokuwa na ndugu na jamaa zake anakuwa tayari kuwaambia kama mnataka huduma fulani, nendeni sehemu fulani(yaani kwako). Hii ni njia bora (more…)