Category Archives: BIASHARA NA UJASIRIAMALI

Hatua tatu muhimu za safari ya ujasiriamali.

By | October 27, 2014

Mara nyingi tumekuwa tukiona wajasiriamali waliofanikiwa na sisi kutamani sana kufikia mafanikio kama hayo. Kila siku tumekuwa tunapata hadithi mbalimbali za watu ambao walianzia chini kabisa ila baada ya muda wameweza kufikia mafanikio makubwa sana kupitia ujasiriamali. Ni hadithi za aina hii ambazo zinatufanya tuone inawezekana kupata mafanikio makubwa sana (more…)

Maswali matatu muhimu ya kujiuliza kuhusu soko.

By | October 20, 2014

Mafanikio yako wewe kwenye ujasiriamali yanatokana na mambo mengi sana. Moja ya jambo muhimu litakalokuletea mafanikio makubwa ni kulijua soko lako vizuri na jinsi ya kulifikia soko hilo. Na ili kufanikiwa kwa kiwango kikubwa sana unatakiwa uweze kulitawala soko kwa kiwango cha kutosha kuifanya biashara yako ipate faida kubwa na (more…)

Vitu vitatu muhimu kwa kila mjasiriamali kujifunza.

By | October 13, 2014

Mafanikio kwenye ujasiriamali sio bahati bali ni kitu kinachoweza kufanyiwa kazi na kila mjasiriamali. Kila mjasiriamali anaweza kufikia mafanikio makubwa kuliko aliyonayo sasa, kama atakuwa tayari kujifunza zaidi na kufanya kazi kwa bidii na maarifa zaidi. Ukichunguza kwa makini wajasiriamali waliofanikiwa utaona ni watu wa kujifunza na wako makini na (more…)

Huu ni wakati mzuri sana wa wewe kuwa mjasiriamali.

By | October 6, 2014

Katika historia ya dunia haijawahi kutokea wakati mzuri wa kuwa mjasiriamali kama ilivyo sasa. Tunaishi kwenye zama ambazo mtu yeyote anaweza kuingia kwenye ujasiriamali na kupata mafanikio makubwa sana. Katika karne ya 19 na karne ya 20, ili kufanikiwa kwenye ujasiriamali ilibidi mtu awe na uwezo wa kujenga na kumiliki (more…)

Ukweli halisi kuhusu safari ya ujasiriamali.

By | September 29, 2014

Katika nyakati hizi ujasiriamali umekuwa ukizungumziwa sana katika jamii zetu. Mafunzo memgi ya ujasiriamali yametolewa na watu wengi sana wamehamasika kuingia kwenye ujasiriamali. Vyombo vya habari navyo vimeupamba sana ujasiriamali. Wajasiriamali wanaoonekana kupata mafanikio makubwa wamekuwa wakitumiwa kama mifano kwenye sehemu mbalimbali. Kila siku tunasikia habari kwamba mtu alianza na (more…)

Njia tano unazoweza kutumia kuongeza kipato chako kwenye biashara.

By | September 22, 2014

Moja ya changamoto ambazo zinawakabili wajasiriamali wengi ni kipato kidogo kutoka kwenye ujasiriamali wao au biashara zao. Watu wengi wamekuwa kwenye ujasiriamali kwa muda mrefu ila hawaoni mabadiliko makubwa kwenye kipato chao. Hali hii imefanya biashara za watu wengi kudumaa na hatimaye kufa kabisa. Leo tutajadili njia tano unazoweza kutumia (more…)

Je ufanye ujasiriamali au biashara ya aina gani? Jibu utalipata hapa.

By | September 15, 2014

Katika moja ya maswali ambayo huwa napata kutoka kwa wasomaji wengi ni mtu afanye ujasiriamali wa aina gani? Au wengine huuliza nina kiasi fulani cha mtaji, naomba unishauri nifanye biashara gani? Hili ni swali ambalo linawasumbua watu wengi sana na kukosekana kwa ushauri mzuri kumewafanya watu wengi kufanya maamuzi ambayo (more…)

Sifa tatu za wajasiriamali wenye mafanikio makubwa.

By | September 8, 2014

Mabadiliko makubwa duniani yameletwa na wajasiriamalia au watu wenye mawazo ya kijasiriamali. Hii ni kwa sababu watu hawa wanakuwa na mawazo tofauti ukilinganisha na watu wengine kwenye jamii. Wajasiriamali wanaiona dunia tofauti na ile inayoonekana na watu wengine na ndio maana huja na ugunduzi unaobadili maisha ya watu wengi sana. (more…)

Hisia mbili zinazowaongoza binadamu na jinsi ya kuzitumia kwenye biashara na ujasiriamali.

By | September 1, 2014

Mafanikio kwenye ujasiriamali yanatokana na vitu vingi sana. Ni muhimu sana kujifunza mambo yote yatakayokuletea mafanikio ili uweze kufikia mafanikio makubwa kupitia ujasiriamali. Leo tutaona hisia mbili zinazowaongoza au kuwatawala binadamu na jinsi unavyoweza kuzitumia kufikia mafanikio makubwa sana. Wakati mwingine tutajifunza mambo mengine yatakayokuletea mafanikio makubwa. Hisia ya kwanza; (more…)

Mambo Matano Yanayowazuia Wajasiriamali Wengi Kufikia Mafanikio Makubwa.

By | August 25, 2014

Unapokuwa mjasiriamali hakuna kiwango cha mwisho cha mafanikio unachoweza kufikia, hii ina maana kwamba unaweza kufikia mafanikio makubwa zaidi ya hayo uliyonayo sasa. Tofauti na mwajiriwa ambaye mshahara wake unajulikana na hata ka autaongezeka ni kidogo sana, mjasiriamali unapanga kipato chako mwenyewe na hivyo unaweza kukiongeza bila ya kuomba au (more…)