#SheriaYaLeo (260/366); Waondoe kwenye upande hasi.

By | July 18, 2022

#SheriaYaLeo (260/366); Waondoe kwenye upande hasi. Ni rahisi kukaa upande hasi kuliko upande chanya. Ni rahisi kukosoa watu kuliko kuwasifia. Ndiyo maana watu wengi huwa wanakimbilia kwenye huo upande hasi. Inahitaji jitihada kubwa kukaa upande chanya na kueleza ubora wa kitu. Ni rahisi kukaa upande hasi na kuonyesha udhaifu wa (more…)

2755; Unakimbilia wapi?

By | July 17, 2022

2755; Unakimbilia wapi? Hebu pata picha unapita njiani na kukutana na mtu unayemfahamu, anatembea kwa haraka sana. Unamsimamisha ili kumsalimia anakujibu kwa haraka na kuendelea na kasi yako, anakuambia anataka kuwahi. Unamuuliza kwani unawahi wapi? Anakujibu hata sijui, ila nataka tu kuwahi. Je utamwelewaje mtu wa aina hii? Ni dhahiri (more…)

#SheriaYaLeo (259/366); Achana na mazoea.

By | July 17, 2022

#SheriaYaLeo (259/366); Achana na mazoea. Majenerali bora wa kivita na wanamikakati wabunifu huwa wanafanikiwa siyo kwa sababu ya ujuzi walionao, ila kwa sababu wanaweza kuachana na mazoea na kuweka umakini wao kwenye wakati uliopo. Hivyo ndivyo ubunifu unavyochochewa na fursa kutumiwa. Maarifa, ujuzi na uzoefu huwa vina ukomo. Hakuna kiwango (more…)

2754; Muda wa kazi na muda unaofanya kazi.

By | July 16, 2022

2754; Muda wa kazi na muda unaofanya kazi. Hakuna eneo ambalo watu wengi huwa wanajidanganya kama kwenye muda. Na usipokuwa mkweli kwenye muda wako mwenyewe, hakuna namna unaweza kufanikiwa. Watu wawili, wanaweza kufanya kitu cha aina moja na kuonekana wakiwa na muda unaolingana. Bado mmoja akafanikiwa zaidi ya mwingine. Tofauti (more…)

#SheriaYaLeo (258/366); Usitaharuki.

By | July 16, 2022

#SheriaYaLeo (258/366); Usitaharuki. Huwa ni kawaida yetu sisi binadamu kutaharuki pale tunapokutana na mambo makubwa na ya tofauti na tulivyozoea. Lakini kutaharuki huko huwa hakuna msaada wowote, zaidi ya kutufanya tuwe dhaifu zaidi na kuwa kwenye hali ya kushindwa. Jambo lolote linalotokea, hata liwe kubwa na la tofauti kiasi gani, (more…)

#SheriaYaLeo (257/366); Fikiria matokeo yasiyotegemewa.

By | July 15, 2022

#SheriaYaLeo (257/366); Fikiria matokeo yasiyotegemewa. Sisi binadamu, huwa tunafikiri kwa uvivu na urahisi. Huwa tunaona kama vile matokeo yanafuatana. Kwamba baada ya A ni B, kisha C na kuendekea, sivyo mambo yanavyokuwa kwenye uhalisia. Unapaswa kujua kwamba kila jambo hapa duniani lina ugumu na utata. Kuna mambo yatahusishwa ambayo hayakutegemewa (more…)

2752; Niseme vibaya kwenye mengine yote, lakini siyo kwenye hiki kimoja.

By | July 14, 2022

2752; Niseme vibaya kwenye mengine yote, lakini siyo kwenye hiki kimoja. Kama binadamu, najua sijakamilika. Nina maeneo ambayo nina uimara mkubwa. Na maeneo ambayo nina udhaifu mkubwa. Najua kuna watu wananisema vibaya kwenye mambo mbalimbali, mengine ya kweli na mengine siyo ya kweli. Wapo wanaoweza kuwa wanasema sijali, nina roho (more…)

#SheriaYaLeo (256/366); Muda ndiyo kitu pekee ulichonacho.

By | July 14, 2022

#SheriaYaLeo (256/366); Muda ndiyo kitu pekee ulichonacho. Muda ni rasilimali muhimu sana uliyonayo kwenye maisha yako. Kuweza kutumia muda wako vizuri kunakufanya uweze kufanya makubwa zaidi. Ili kuweza kunufaika vizuri na muda, lazima uuchukulie kwa tofauti na ambavyo umekuwa unauchukulia. Kiuhalisia, tangu siku uliyozaliwa, muda ndiyo kitu pekee ulichonacho. Ndiyo (more…)

2751; Kujua, kuweza na kufanya.

By | July 13, 2022

2751; Kujua, kuweza na kufanya. Kama leo hii, utaacha kabisa kujifunza vitu vipya, yaani usijifunze chochote kipya, ila ukafanyia kazi yale ambayo tayari unayajua, bado utapata mafanikio makubwa sana. Kwa mfano ukaweka juhudi kubwa kwenye kazi/biashara yako kila mara. Ukawa na matumizi madogo kuliko kipato chako na hivyo kuweka akiba (more…)