#SheriaYaLeo (170/366); Usifanye mabadiliko makubwa kwa wakati mmoja.

By | April 19, 2022

#SheriaYaLeo (170/366); Usifanye mabadiliko makubwa kwa wakati mmoja. Sisi binadamu huwa tunapenda kusikia kuhusu mabadiliko, ila huwa hatupo tayari kubadilika. Watu wanajua kabisa umuhimu wa mabadiliko kwenye taasisi na hata mtu mmoja mmoja. Lakini pale mabadiliko hayo yanapowahusu wao binafsi na kuathiri maslahi yao huwa hawayafurahii. Mabadiliko ni mazuri na (more…)

2665; Unahitaji watu wa kukusukuma.

By | April 18, 2022

2665; Unahitaji watu wa kukusukuma. Pamoja na magumu na changamoto mbalimbali za dunia, bado asili ya binadamu huwa ina nguvu sana. Kwa mfano, ni asili yetu binadamu kuridhika na kile ambacho tayari tumeshakipata. Pamoja na kwamba dunia inabadilika na chochote kinachoturidhisha sasa hakiwezi kuturidhisha kesho, bado hatuwezi kulivuka hilo peke (more…)

#SheriaYaLeo (169/366); Tumia mwonekano kushawishi.

By | April 18, 2022

#SheriaYaLeo (169/366); Tumia mwonekano kushawishi. Watu huwa wanashawishika sana na mwonekano wa vitu ulivyo. Vitu kama rangi, muundo na mpangilio wa vitu vina nguvu ya kuwashawishi watu kwa namna fulani. Kwa mfano matumizi ya rangi nyekundu kwenye maandishi yanawafanya watu waone kitu ni muhimu na cha haraka hivyo kushawishika kuchukua (more…)

2664; Ni wewe umewafundisha.

By | April 17, 2022

2664; Ni wewe umewafundisha. Kama watu wanakuchukulia kwa namna ambayo hupendezwi nayo, wao siyo wa kulaumu, bali wewe ndiye wa kujilaumu. Kwani kwa vyovyote vile watu wanavyokuchukulia, ni wewe umewafundisha. Wewe ndiye umewaonyesha na kuwaruhusu kwa namna gani wanaweza kukuchukulia. Kama watu wanakudharau, ni kwa sababu umewaonyesha ni sawa wao (more…)

#SheriaYaLeo; (168/366); Dhibiti machaguo unayowapa watu.

By | April 17, 2022

#SheriaYaLeo; (168/366); Dhibiti machaguo unayowapa watu. Watu huwa wanapenda kuona wana uhuru wa kuchagua mambo yao wenyewe. Lakini machaguo yanapokuwa mengi, huwa inakuwa vigumu kwa mtu kuweza kuchagua. Anajikuta njia panda na kushindwa kuchagua kitu kimoja. Ili kuwasaidia watu kufanya maamuzi na wewe kuweza kupata kile unachotaka, dhibiti machaguo unayowapa (more…)

2663; Ambacho hutumii nguvu kufanya.

By | April 16, 2022

2663; Ambacho hutumii nguvu kufanya. Watu wamekuwa wanajiuliza sana ni njia ipi rahisi ya kufanikiwa. Ni kipi ambacho wakifanya watafanikiwa. Wamekuwa wakiwaangalia wale waliofanikiwa kwenye yale wanayoyafanya na kujaribu kuyaiga. Lakini bado hawafanikiwi. Hawafanikiwi kwa sababu wanajaribu kuiga vitu vya nje, Wakati mafanikio yanatokana na vitu vya ndani. Mengi yameandikwa (more…)

#SheriaYaLeo (167/366); Tumia sanaa ya kuwepo na kutokuwepo.

By | April 16, 2022

#SheriaYaLeo (167/366); Tumia sanaa ya kuwepo na kutokuwepo. Unapaswa kujua jinsi ya kupangilia kuwepo na kutokuwepo kwako. Sisi binadamu huwa tunadharau kitu kinachopatikana muda wote na kuthamini kile ambacho hakipatikani. Kwa ujumla, ni vyema kuegemea zaidi upande wa kutokuwepo/kutokupatikana ili pale unapokuja kuonekana watu wanakuwa na shauku kubwa. Ukifanya hilo, (more…)

2662; Kama Ninge….

By | April 15, 2022

2662; Kama Ninge…. Hakuna njia rahisi ya kuyaharibu maisha yako na kujizuia kufanikiwa kama kuwa na majuto. Kuangalia yale ambayo hukufanya au hukuchagua na kuona labda ndiyo yangekuwa bora ni uhakika unachofanya sasa hakiwezi kuwa bora. Uliacha kazi na kuingia kwenye biashara, lakini mambo hayaendi kama ulivyotegemea. Unaweza kujiambia, kama (more…)

#SheriaYaLeo (166/366); Kuwa mkali.

By | April 15, 2022

#SheriaYaLeo (166/366); Kuwa mkali. Mara nyingi huwa tunapenda kuwa wapole na wenye kujali wengine ili kuweza kuendana nao vizuri na kupata kile tunachotaka. Hili huwa linafanya kazi vizuri wakati wa kawaida. Lakini wakati wa hatari hilo linakuwa mzigo kwako, kufanya hivyo kunapelekea watu wakuone ni mtu unayefaa kuonewa, kukatishwa tamaa (more…)

2661; Wanakuvuruga usione uhalisia.

By | April 14, 2022

2661; Wanakuvuruga usione uhalisia. Mpishi mmoja mbobezi amewahi kusema njia ya haraka ya kujua kama chakula ni kizuri au kibaya ni kuangalia viungo ambavyo vimewekwa kwenye chakula hicho. Akaendelea kusema unapoona chakula kina viungo vingi sana, jua siyo kizuri. Hivyo wanaweka viungo vingi ili kukuvuruga usione uhalisia. Alitumia maneno makali (more…)