Category Archives: SHERIA ZA SIKU

#SheriaYaLeo (183/366); Iangalie dunia kwa jicho la ushawishi.

By | May 2, 2022

#SheriaYaLeo (183/366); Iangalie dunia kwa jicho la ushawishi. Ili kuweza kuwa na nguvu ya ushawishi huhitaji kuwa na mabadiliko makubwa kwenye tabia au mwonekano wako. Ushawishi ni mchezo wa kisaikolojia na hivyo kila mtu anaweza kuwa na ubobezi kwenye mchezo huu. Kinachohitajika ni uiangalie dunia kwa utofauti, kupitia jicho la (more…)

#SheriaYaLeo (182/366); Weka wazi mbinu zako.

By | May 1, 2022

#SheriaYaLeo (182/366); Weka wazi mbinu zako. Pamoja na kwamba ni muhimu kutumia mbinu mbalimbali kuficha nia yako halisi, kuna wakati utalazimika kuweka mbinu na nia yako wazi. Pale watu wanapojua kwamba huwa unatumia mbinu mbalimbali kuficha nia yako, hilo linakosa nguvu. Kwani inakuwa vigumu kwao kuendelea kukuamini. Ni katika hali (more…)

#SheriaYaLeo (181/366); Iga Maadili Yao.

By | April 30, 2022

#SheriaYaLeo (181/366); Iga Maadili Yao. Kufikiri na kusema kile unachotaka kusema kwa watu wote ni kukitafutia matatizo yasiyo na manufaa. Watu wenye hekima wanajua kwamba wanapaswa kuonyesha tabia zinazoendana na wale wanaowazunguka. Wanajua siyo lazima waamini kwenye mambo hayo. Manufaa wanayopata ni kwa kufanya kile ambacho wengine wanafanya kwa nje, (more…)

#SheriaYaLeo (180/366); Tengeneza upya nguvu ya mamlaka yako.

By | April 29, 2022

#SheriaYaLeo (180/366); Tengeneza upya nguvu ya mamlaka yako. Unaweza kujenga mamlaka yako au mafanikio na kufika viwango vya juu kabisa. Lakini kadiri muda unavyokwenda, mamlaka hayo yanaanza kupoteza nguvu zake. Watu wanakuzoea kwa yale ambayo tayari umekuwa unayafanya. Na huku watu wapya wanaokuja wakiwa hawakujui vyema. Wewe mwenyewe unakuwa unafanya (more…)

#SheriaYaLeo (179/366); Waambie watu wanachotaka kusikia.

By | April 28, 2022

#SheriaYaLeo (179/366); Waambie watu wanachotaka kusikia. Ukweli huwa unauma, Watu wengi huwa hawapendi kusikia ukweli. Hivyo kama unataka kupata wafuasi wengi, usiwaambie watu ukweli, bali waambie kile wanachotaka kusikia. Watu hawataki kusikia kwamba kujenga utajiri kunahitaji muda, juhudi na nidhamu ya hali ya juu. Wanataka kusikia wakipanda pesa leo kesho (more…)

#SheriaYaLeo (178/366); Kamwe usifanye kwa mazoea.

By | April 27, 2022

#SheriaYaLeo (178/366); Kamwe usifanye kwa mazoea. Unapokuwa kijana huwa ni rahisi kuchukua hatua za tofauti. Japo zinaweza kuwa hatari, lakini ndiyo zinazoleta matokeo makubwa na ya tofauti. Lakini kadiri umri unavyokwenda, unaanza kufanya zaidi kwa mazoea badala ya kujaribu vitu vipya. Kutokana na umri kwenda, unaepuka hatua ambazo ni hatari (more…)

#SheriaYaLeo (177/366); Tengeneza hali ya usiri.

By | April 26, 2022

#SheriaYaLeo (177/366); Tengeneza hali ya usiri. Watu wanapoelewa na kuzoea mtu au kitu huwa wanakidharau. Hiyo ni kwa sababu hakuna chochote kinachokuwa kinawasukuma kufuatilia ili kujua zaidi. Kama unataka watu wakufuatilie, tengeneza hali ya usiri. Fanya mambo ambayo watu hawayaelewi au hawawezi kuyaelezea. Kuwa na mwonekano wa tofauti ambao watu (more…)

#SheriaYaLeo (176/366); Tumia maneno matupu.

By | April 25, 2022

#SheriaYaLeo (176/366); Tumia maneno matupu. Watu huwa wanapenda na hata kuelewa zaidi lugha ya picha. Hiyo ni kwa sababu inawawezesha kujenga taswira ya kitu na kukielewa vizuri. Unapotaka kuwahadaa watu, nenda kinyume na hilo. Tumia lugha ya maneno matupu ambayo hayamwezeshi mtu kujenga taswira yoyote. Lugha ya aina hiyo inamfanya (more…)

#SheriaYaLeo (175/366); Jinsi ya kuwafanya watu wawe tayari kukusaidia.

By | April 24, 2022

#SheriaYaLeo (175/366); Jinsi ya kuwafanya watu wawe tayari kukusaidia. Kama unataka watu wakusaidie kitu fulani, usiwakumbushe jinsi ambavyo wewe umewahi kuwasaidia huko nyuma. Unaweza kudhani kwa kuwakumbusha hilo wataona wanapaswa kulipa fadhila na hivyo kusukumwa kukusaidia. Lakini siyo kinachotokea. Unapowakumbusha watu jinsi ulivyowasaidia huko nyuma unawafanya wajione hawajiwezi na wanategemea (more…)

#SheriaYaLeo (174/366); Dhibiti kile unachosema.

By | April 23, 2022

#SheriaYaLeo (174/366); Dhibiti kile unachosema. Mamlaka ni mchezo wa mwonekano kadiri unavyozungumza kidogo, ndivyo unavyoonekana wa muhimu na mwenye mamlaka makubwa. Unapokaa kimya unawafanya wengine washindwe kukutabiri. Maana sisi binadamu ni mashine za kutengeneza maana, huwa hatuwezi kutulia kama hatujui maana au nia ya kitu fulani. Unapozungumza sana, unaweka kila (more…)