#SheriaYaLeo (330/366); Geuza upendo binafsi kuwa huruma.

By | September 26, 2022

#SheriaYaLeo (330/366); Geuza upendo binafsi kuwa huruma. Huwa tunadhani tunawaelewa vizuri watu tunaojihusisha nao. Maisha yanaweza kuwa magumu na tuna majukumu mengi ya kukamilisha. Pia tu wavivu na tunapendelea kuwahukumu watu kwa mazoea. Lakini hayo yote siyo sahihi. Mafanikio yetu kwenye maisha yanategemea sana uwezo wetu wa kuwasoma na kuwaelewa (more…)

2825; Unamtoa mtu.

By | September 25, 2022

2825; Unamtoa mtu. Kwenye maisha, kila mtu tayari ana mtu wake. Hivyo unapotaka kupata mtu, inabidi uwe tayari kumtoa aliyepo. Twende kwenye mfano ili tuelewane. Kama upo kwenye biashara, wateja unaowalenga tayari wana pengine wanaponunua hicho unachouza. Ili uwapate waje kununua kwako, lazima uwatoe kule walipo sasa. Siyo rahisi kumtoa (more…)

#SheriaYaLeo (329/366); Kaa kwenye kundi sahihi.

By | September 25, 2022

#SheriaYaLeo (329/366); Kaa kwenye kundi sahihi. Dhumuni la makundi mbalimbali ni kukamilisha majukumu, kufanya kazi, kutatua matatizo. Makundi yanakuwa na rasilimali muhimu ambazo zikitumika vizuri zinakuwa na tija kubwa. Lakini pia ndani ya kundi huwa kuna ushindani baina ya watu, ambao unaweza kuwasukuma watu kufanya zaidi. Kundi lenye afya huwa (more…)

2824; Hakuna kushindwa.

By | September 24, 2022

2824; Hakuna kushindwa. Kitu kinachoitwa kwenye maisha hakipo kiuhalisia. Bali ni msamiati ulitengenezwa na jamii ili kuwadhibiti watu. Tunapoiangalia asili kwa namna inavyofanya kazi, tunaona wazi kabisa kushindwa hakupo. Kwenye eneo moja, panda mbegu za papai na embe. Siku chache mbegu za papai zitakuwa zimeota, ila mbegu za embe zitakuwa (more…)

#SheriaYaLeo (328/366); Sifia ukuu wa watu.

By | September 24, 2022

#SheriaYaLeo (328/366); Sifia ukuu wa watu. Kusifia ni kinyume na wivu – tunatambua mafanikio ya watu na kuyafurahia bila ya kujisikia vibaya. Tunakubali ubora wao kwenye sanaa au sayansi au biashara bila ya kupata maumivu. Hilo linaenda zaidi, katika kutambua ukuu wa wengine, tunasherekea uwezo wa juu kabisa wa jamii (more…)

2823; Tayari najua.

By | September 23, 2022

2823; Tayari najua. Hayo ni maneno ambayo yamewapoteza wengi sana na kuwazuia wasifanikiwe. Ni maneno ambayo yamewazuia wengi wasiendelee kujifunza na kuwa bora zaidi. Kila mtu hudhani tayari anajua mengi, lakini kiuhalisia hana uelewa kama anavyodhani anao. Kujifunza kitu chochote kile, kunahitaji marudio ya muda mrefu. Hata pale unapodhani tayari (more…)

#SheriaYaLeo (327/366); Pokea kila kinachokuja kwako.

By | September 23, 2022

#SheriaYaLeo (327/366); Pokea kila kinachokuja kwako. Kwenye safari yako ya maisha, kuna mengi yatakuja kwako ambayo ni tofauti kabisa na mategemeo yako. Kwenye hali kama hiyo ni rahisi sana kulalamika na kulaumu wengine kwa hayo unayokuwa unapitia. Lakini kufanya hivyo hakutasaidia chochote. Utaendelea kubaki kwenye hali hiyo hiyo. Kitu pekee (more…)

2822; Umalaya wa fursa.

By | September 22, 2022

2822; Umalaya wa fursa. Richard Branson amewahi kunukuliwa akisema fursa za biashara ni kama daladala, ukikosa moja, kuna jingine linakuja. Kwa maana rahisi ni kwamba fursa ni nyingi na haziishi. Lakini wanachokifanya walio wengi ni kutaka kupanda kila daladala. Pata picha umeenda kituo cha daladala, ikaja daladala ukaipanda, lakini kabla (more…)

#SheriaYaLeo (326/366); Ungana na kilicho karibu yako.

By | September 22, 2022

#SheriaYaLeo (326/366); Ungana na kilicho karibu yako. Maisha ni mafupi na nguvu zetu zina ukomo. Kwa kuongozwa na tamaa zetu, tunaweza kupoteza muda na nguvu kwenye kutafuta mabadiliko. Kwa ujumla, hupaswi kusubiri na kutumaini mambo yatakwenda vizuri, bali unapaswa kutumia vizuri kile ulichonacho. Asili inakuunga mkono. Kwa kuzamisha akili yako (more…)

2821; Kila mtu anafanya.

By | September 21, 2022

2821; Kila mtu anafanya. Sababu ya hovyo kabisa ya kufanya kitu ni kila mtu kuwa anakifanya. Sisi binadamu kama viumbe wa kimamii huwa tunapenda sana kufuata mkumbo. Lakini tuanze tu kwa kuuangalia ukweli ulivyo. Watu wengi kwenye jamii hawafanikiwi. Kwa kuwa wale tunaojihusisha nao wana ushawishi mkubwa kwetu, tunapaswa kuwaepuka (more…)