Author Archives: Dr. Makirita Amani

About Dr. Makirita Amani

Dr. Makirita Amani ni daktari wa binadamu, mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali. Dhumuni lake kubwa kwenye maisha ni KUWASAIDA WATU KUBORESHA MAISHA YAO NA KUFIKIA MAFANIKIO MAKUBWA KUPITIA KAZI ANAZOFANYA. Mawasiliano 0717396253 email makirita@kisimachamaarifa.co.tz

#SheriaYaLeo (316/366); Panda mlima.

By | September 12, 2022

#SheriaYaLeo (316/366); Panda mlima. Kwa sisi binadamu, kukaa kwenye wakati uliopo ni kama kuishi sehemu ya chini ya mlima. Kile kinachoonekana kwa macho ndiyo kinaathiri maamuzi yetu. Kupita kwa muda ni sawa na kupanda mlima. Muda unapopita, tunakuwa hatuna tena hisia ambazo zilituathiri kwenye wakati husika. Tunaweza kujitenga na tukio (more…)

2811; Kinachohitajika ni furaha.

By | September 11, 2022

2811; Kinachohitajika ni furaha. Tunahangaika na mambo mengi kwenye maisha yetu. Lakini mwisho wa siku kinachohitajika ni furaha. Huenda hatujui moja kwa moja, lakini kila tunachofanya, msingi wake ni furaha. Sasa kwa kutokujua chanzo sahihi cha furaha, tunajikuta tunajaribu kila aina ya kutu kuona kama kitatupa furaha. Kubahatisha furaha imekuwa (more…)

#SheriaYaLeo (315/366); Vuka ukabila.

By | September 11, 2022

#SheriaYaLeo (315/366); Vuka ukabila. Ukabila una mizizi ndani ya asili ya binadamu. Ulitusaidia sana kipindi ambacho usalama wa mtu ulitegemea sana kuwepo ndani ya kundi. Kuwa nje ya kundi ilikuwa hatari kubwa kwa maisha ya mtu yeyote. Lakini kwa sasa mambo yamebadilika, hali ya usalama ni kubwa na hakuna hatari (more…)

2810; Usitengeneze majuto.

By | September 10, 2022

2810; Usitengeneze majuto. Unakumbuka ukiwa shuleni, kuna wakati ulikuwa husomi sana na pale matokeo yalipokuwa yanatoka ukawa unajiambia kama ungeweka juhudi zaidi, ungeweza kupata matokeo zaidi? Hiyo ni dhana ambayo wengi wanaondoka nayo shuleni na kwenda nayo kwenye maisha, kitu kinachowazuia wasipate mafanikio makubwa. Kufanya vitu nusu nusu ili ukishindwa (more…)

#SheriaYaLeo (314/366); Dhibiti hisia zako za majigambo.

By | September 10, 2022

#SheriaYaLeo (314/366); Dhibiti hisia zako za majigambo. Majigambo ni nguvu ambayo ipo ndani ya kila mmoja wetu. Nguvu hiyo inatusukuma kutaka kutaka vitu zaidi ya tulivyonavyo, kutambulika na wengine na kuunganika na kitu kikubwa. Tatizo halipo kwenye nguvu yenyewe, kwani inaweza kutumika kuchochea matamanio yetu. Tatizo lipo kwenye kudhibiti nguvu (more…)

2809; Rahisi kufanya.

By | September 9, 2022

2809; Rahisi kufanya. Ukichunguza kwa makini, utagundua kwamba matatizo yote ambayo umewahi kuwa nayo kwenye maisha, chanzo chake ni kukimbilia vitu rahisi kufanya. Hii ni asili yetu binadamu, huwa hatupendi vitu vigumu. Hivyo kila mara tunatafuta kilicho rahisi. Na huko pia ndipo tunapotengeneza matatizo mengi tunayokuwa nayo kwenye maksha. Hata (more…)

#SheriaYaLeo (313/366); Uvumilivu mkuu.

By | September 9, 2022

#SheriaYaLeo (313/366); Uvumilivu mkuu. Muda ni dhana ambayo sisi binadamu tumeitengeneza ili kuweza kuvumilia hali ya ulimwengu usio na ukomo. Kwa kuwa tumetengeneza muda wenyewe, tuna nguvu ya kuweza kuuathiri, kucheza nao kwa namna fulani. Tukiwa watoto, muda unaonekana mrefu na unaoenda taratibu. Lakini tukiwa watu wazima, muda unaonekana mfupi (more…)

2808; Kujua hujui.

By | September 8, 2022

2808; Kujua hujui. Kujua hujui ndiyo ujuzi muhimu ambao utakusaidia sana kwenye maisha yako. Utakufanya uwe mnyenyekevu na tayari kujifunza ili kuwa bora zaidi na kuweza kupiga hatua kubwa. Na hili siyo rahisi kukubali na hata kulifanya. Huwa tuna ufahari wa kutaka kuwaonyesha wengine kwamba tunajua. Huwa tunaona kuonekana hatujui (more…)

#SheriaYaLeo (312/366); Furahia mafanikio ya wengine.

By | September 8, 2022

#SheriaYaLeo (312/366); Furahia mafanikio ya wengine. Ni rahisi kwetu binadamu kupata wivu pale wengine wanapofanikiwa kuliko sisi. Na pale watu hao tunaowaonea wivu wanapopatwa na matatizo, huwa tunafurahia. Tunafurahia kuwaona wakiwa kwenye matatizo na maumivu mbalimbali. Lakini hilo halina faida yoyote kwetu, zaidi tu ya kutufanya tushindwe kufanikiwa kama watu (more…)

2807; Unahangaika na mambo mengi sana.

By | September 7, 2022

2807; Unahangaika na mambo mengi sana. Mwanga wa jua, ukitawanyika, unaishia kuangaza tu. Lakini mwanga huo huo ukikusanywa sehemu moja, unakuwa na nguvu ya kuchoma. Hivyo pia ndivyo ilivyo kwenye nguvu zetu binafsi, tukizitawanya kwenye mambo mengi, tunaishia kupata matokeo ya kawaida. Lakini tukikusanya nguvu hizo kwenye jambo moja au (more…)